Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Ulaji wa chakula maarufu ‘chips’ umeelezwa kuwa hatai kwa wajawazito kwani huchochea kwa asilimia 80 ya mama kujifungua mtoto mwenye tatizo la kichwa kikubwa na mgongo wazi.

Chakula kingine kinachochangia hali hiyo ni ulaji wa vyakula vya viwandani.

Hayo yalielezwa juzi na Mtaalamu wa Masuala ya Lishe wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Denis Mbinga alipozungumza na matukionamaisha hospitalini hapo.

Alisema matatizo ya watoto kuzaliwa na vichwa vikubwa, mgongo wazi na magonjwa mengineyo katika siku za karibuni yameongezeka kutokana na ulaji wa vyakula visivyofaa hasa vile vya kusindika na kuacha vya asili vilivyoliwa na wazee wa zamani.

“Kwa kawaida kuna milo mikuu mitatu ambayo tunatakiwa kuipata asubuhi, mchana na jioni. Mlo kamili ni lazima uzingatie vyakula kutoka kwenye makundi makuu matano ambayo ni yale ya nafaka, mizizi na ndizi mbivu, vyakula vyenye asili ya wanyama, mbogamboga, matunda aina zote, mafuta na sukari.

“Katika makundi haya mwili hupata nishati lishe, protini ambayo hujenga mwili, vitamin na madini ambayo hulinda mwili pamoja na kuupa mwili joto,” alisema.

Alisema hata hivyo wengi wanashindwa kuzingaia kula mlo kamili kwa kuzingatia makundi hayo ya vyakula aliyoyataja.

“Katika nchi zilizoendelea watu wanapohitaji kupata watoto huzingatia suala la lishe miezi mitatu kabla huku kwetu barani Afrika hili ni tatizo kwani asilimia kubwa ya wanawake hujikuta tayari wakiwa wajawazito bila ya kujiandaa kuubeba,” alisema.

Naye Elizabeth Lyimo ambaye pia ni mtaalamu wa kitengo hicho pia aliwashauri wanawake kuwahi mapema kliniki ili kufuatilia mwenendo wa afya zao na watoto waliowabeba tumboni.

“Hii itasaidia kubaini mapema kama kuna tatizo lakini kama wakichelewa hatari huwa kubwa zaidi ya kupata watoto wenye matatizo hayo pamoja na udumavu,” alisema.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement