Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
 

Ni wazi sasa uhamasishaji juu ya kuepuka matumizi ya uvutaji wa sigara yamefikia pazuri kufuatia ujumbe wa mwaka huu usemao“jiandae kwa pakiti zisizo na matangazo wala vivutio”   

Kufuatia ujumbe huo, jamii imehamasishwa kujiepusha au kujikinga na vivutio mbalimbali vya matangazo yanayohamasisha matumizi ya sigara ambayo ina madhara makubwa kiafya.

Rai imetolewa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu katika taarifa yake kwa vyombo vya habari juu ya Siku ya Kupinga Matumizi ya Tumbaku Duniani yaliyohadhimishwa leo duniani kote.

“Tanzania kama zilivyo nchi nyingine duniani inaadhimisha siku hii, kwa Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kutoa elimu ya umuhimu wa kuzuia na kujikinga na matumizi ya sigara na bidhaa za tumbaku,” amesema. 

Amesema tafiti nyingi zinathibitisha madhara yatokanayo na matumizi ya tumbaku ni pamoja na magonjwa yasiyoambukiza  kama vile saratani, magonjwa ya mishipa ya damu na moyo, kiharusi, magonjwa ya njia ya hewa.

“Tafiti pia zinaonyesha takriban watu 6,000,000 hupoteza maisha duniani kwa mwaka kwa utumiaji wa tumbaku na bidhaa zake,” amesema.

Waziri Ummy amesema kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya kupinga matumizi ya tumbaku duniani kwa mwaka 2016, inalenga kuelimisha na kuhamasisha jamii kuachana na matumizi ya tumbaku na kusisitiza kwa wazalishaji kutokuweka maandishi au nembo zinazovutia ili kuishawishi jamii kutumia bidhaa hizo. 

“Tumbaku imekuwa ikisababisha madhara kiafya kama vile magonjwa mbalimbali yasiyoambukiza. Magonjwa hayo ni magonjwa ya moyo na mishipa ya damu, saratani, ugonjwa wa kisukari na magonjwa ya njia ya hewa,” amesema.

Siku ya kupinga matumizi ya Tumbaku Duniani huadhimishwa kila mwaka Mei 31.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement