Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Mmoja wa madaktari wa macho akimpima mwanafunzi wakati wa upimaji huo.
KLABU ya Rotary ya Oysterbay kwa kushirikiana na madaktari wa Hospitali ya Taifa  Muhimbili (MNH), Amana na Mnazi Mmoja wamefanya upimaji afya kwa wanafunzi  1200 wa Shule ya Msingi Msasani A. 

Upimaji huo ulifanyika jana shuleni hapo ambapo pia wazazi wa wanafunzi hao na walimu wa Shule hiyo walipata fursa ya kupima afya zao na kuchangia damu Hospitali ya Taifa Muhimbili. 
 
Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa upimaji huo Mwenyekiti wa Rotary, Mhandisi Mohamed Verse (mwenye kofia) alisema waliguswa kufadhili upimaji huo kwani suala la afya ni jambo la msingi kwa mwanadamu.

“Rotary tumekuwa na utaratibu wa kuisaidia jamii. Hii ni klabu inayoundwa na wafanyabiashara pamoja na wataalamu mbalimbali. Hii si mara ya kwanza kusidaia shule hii, tayari tumeshajenga maktaba mbili, tumeweka maji safi na salama, tumepanda miti, tumejenga ukuta ili kuimarisha ulinzi na awamu hii tumeona ni vyema tufanye upimaji afya,” alisema.

Alisema Rotary wameweza kuendesha upimaji huo wa afya kwa wanafunzi hao kwa kushirikiana na wenzao wa kampuni ya Diamond Trust.

Naye Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Egidius Mjumangoma alisema amefurahishwa na hatua hiyo ya upimaji afya kwani itasaidia kuwatambua na kuwasaidia mapema wale watakaokutwa na ugonjwa.
 
“Watanzania hatuna ule utamaduni wa kupima afya zetu, leo (jana) wanafunzi wangu wamepata fursa ya kupimwa macho, meno, malaria na maradhi mengineyo, hii itasaidia kuwatambua na kuwasaidia mapema wale watakaokutwa na tatizo.

“Nawashukuru mno Rotary maana wamekuwa washirika waaminifu wa vitendo na si maneno pekee, bado tunaomba wadau wengine waige mfano huu na kutusaidia bado tuna changamoto mbalimbali zinatukabili,” alisema.

Naye Mwenyekiti wa Elimu na Malezi wa Kata ya Bonde la Mpunga ambako ipo shule hiyo, Faudhia Kigwe alisema ufadhili wa Rotary katika sekta ya elimu unapaswa kuigwa na kampuni nyinginezo.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement