Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
 
picha hii inaonesha sehemu mbalimbali za mwili wa mwanaume

Na Veronica Romwald, Dar es Salaam

WANAUME ambao korodani zao hazijashuka kwenye mfuko wake wapo hatarini kwani kuna uwezekano mkubwa wa kugeuka kuwa saratani zikiwa tumboni.

Korodani ni kiungo muhimu mno katika mwili wa mwanaume kazi yake kuu ikiwa ni kuzalisha mbegu za kiume pamoja na homoni za kiume (Testosterone).

Daktari Bingwa wa Mfumo wa Njia ya Mkojo (Urolojia) wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Ryuba Nyamsogoro  alisema mapema wiki hii alipozungumza na MTANZANIA kwenye mahojiano maalumu.

“Kawaida mwanaume ana korodani mbili, moja ikiwa upande wa kushoto na nyingine upande wake wa kulia. 

Huwa zinatengenezwa tumboni na baadae hushuka hadi katika vifuko vyake vilivyoko nje ya mwili wa mwanaume karibu na uume.

“Huwa zinatengenezwa ndani ya tumbo la mtoto wa kiume na huanza kushuka kuelekea kwenye vifuko vyake kupitia mrija wake wa Gubanakulamu mimba ikiwa Katika kipindi cha kati ya mwezi wa sita na saba tangu ilipotungwa ,” alisema.

Alisema hata hivyo kuna wakati korodani huwa hazishuki licha ya muda wake wa kushuka kuwa umefika na kwamba hiyo hutokana na matatizo mbalimbali na wapo wengine ambao hujikuta hazishuki zote mbili ingawa hawa ni wachache,” alisema.

Daktari huyo alisema hakuna dalili zozote ambazo mjamzito anaweza kuziona na kujua kuwa mtoto aliyembeba tumboni atakuwa na tatizo hilo siku zijazo.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement