Waziri Ummy akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali hiyo, Profesa Ainory Gessase.
Na.Catherine Sungura ,Dodoma
Serikali kupitia Wizara ya Afya inatarajia kuzindua huduma zote za kiuchunguzi za magonjwa kwenye hospitali ya kisasa ya Benjamin Mkapa iliyopo mjini Dodoma
Hayo yamesemwa leo na waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati alipotembelea hospitali hiyo na kuona inavyoendelea kutoa huduma za afya kwa wananchi
Waziri Ummy alisema serikali imejipanga katika kutekeleza ahadi yake kwa wananchi katika utoaji huduma bora na za kisasa katika hospitali hiyo
"Nawaahidi nitafanya uzinduzi rasmi wa huduma za uchunguzi wa magonjwa ili wananchi waelewe hospitali yetu inatoa huduma zipi ili kila mwananchi atambue nini kinapatikana hapa"alisema Mhe.Ummy
Aidha,Waziri Ummy alisema licha ya kazi nzuri inayofanywa na watoa huduma wa afya wa hospitali hiyo bado inakabiliwa na changamoto kubwa ikiwemo kukatika kwa umeme mara kwa mara na kuahidi kuwasiliana na wizara ya Nishati na Madini ili kutatua tatizo hilo.
Serikali kupitia Wizara ya Afya inatarajia kuzindua huduma zote za kiuchunguzi za magonjwa kwenye hospitali ya kisasa ya Benjamin Mkapa iliyopo mjini Dodoma
Hayo yamesemwa leo na waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati alipotembelea hospitali hiyo na kuona inavyoendelea kutoa huduma za afya kwa wananchi
Waziri Ummy alisema serikali imejipanga katika kutekeleza ahadi yake kwa wananchi katika utoaji huduma bora na za kisasa katika hospitali hiyo
"Nawaahidi nitafanya uzinduzi rasmi wa huduma za uchunguzi wa magonjwa ili wananchi waelewe hospitali yetu inatoa huduma zipi ili kila mwananchi atambue nini kinapatikana hapa"alisema Mhe.Ummy
Aidha,Waziri Ummy alisema licha ya kazi nzuri inayofanywa na watoa huduma wa afya wa hospitali hiyo bado inakabiliwa na changamoto kubwa ikiwemo kukatika kwa umeme mara kwa mara na kuahidi kuwasiliana na wizara ya Nishati na Madini ili kutatua tatizo hilo.
Hata hivyo alisema wizara yake inafuatilia upatikanaji wa fedha kiasi cha
shilingi milioni 137 za kukamilisha ujenzi wa ufungaji wa baadhi ya vifaa tiba
vilivyopo hospitalini hapo na hivyo kuwakaribisha wananchi wote kufika
hospitali hapo kupata huduma za kibingwa za ugonjwa wa kisukari.
Waziri Ummy amesisitiza kuanza kutolewa
kwa huduma za vipimo (kama MRI na CT Scan) katika Hospitali hiyo ili
kuwapunguzia kero wananchi wa mikoa ya kanda ya kati kupata huduma hizo Dodoma
badala ya kusafiri hadi Dar es salaam kupata huduma hizo.
Hospitali ya Benjamin Mkapa ipo katika chuo kikuu cha Dodoma,kwa sasa inahudumia wagonjwa zaidi ya 170 kwa siku,ikikamilika itakua inafanya uchunguzi wa magonjwa ya figo,kisukari pamoja na moyo.
Hospitali ya Benjamin Mkapa ipo katika chuo kikuu cha Dodoma,kwa sasa inahudumia wagonjwa zaidi ya 170 kwa siku,ikikamilika itakua inafanya uchunguzi wa magonjwa ya figo,kisukari pamoja na moyo.
Chapisha Maoni