Yasmin
Eleby akikata keki siku ya harusi yake.
Alichukua uamuzi huo baada ya kukosa mchumba wa kumuoa. Alipanga kwamba mchumba huyo angemuona pindi atakapofikisha umri wa miaka 40.
Alifanya harusi hiyo mwenyewe baada ya kukosa mchumba wa kumuona alipofikisha umri huo na hiyo ni ahadi ambayo aliwahi kuitoa kwamba iwapo atakosekana atajiona mwenyewe akifikisha umri huo kusherehekea miaka yake hiyo. Kitendo ambacho kiliwashangaza wengi.
Duru
zinasema kuwa mwanamke Eleby alifanya harusi yake mwenyewe katika makavazi ya
Houston akiambatana na jamaa na familia yake na wageni wengine waalikwa.
Kwa
sherehe hii, dadake Eleby ndiye aliendesha sherehe hio, kwani ni kinyume na
sheria kwa mtu kujioa mwenyewe. Harusi ya kawaida ni kati ya watu wawili.
Katika
picha za kanisani sherehe ilionekana kuwa ya kawaida bila ya mchumba.
Kulingana
na John Guess Jr afisaa mkuu wa makavazi hayo, sherehe hiyo ilionekana kuwa
bila tashwishi na kuonekana kama jambo la kawaida kwani makavazi hayo
huwakumbatia watu wa jinsia mbali mbali kuendesha harusi zao hapo.
Aliposikia
kwamba Eleby, ambaye anaishi na kufanya kazi ugenini alikuwa anapanga kujioa
mwenyewe, aliharakisha kwenda katika eneo hilo kujionea mwenyewe.
"Eleby
alipofikisha umri wa miaka 40 bila ya kupata mpenzi na mtu mwenye nia ya
kumuoa, aliamua angejioa mwenyewe,''alisema Guess Jr ambaye anasema harusi hiyo
imewashangaza wengi na kuwa gumzo katika mitandao ya kijamii.
Anasema
anakubaliana na Eleby na mtazamo wake wa mapenzi kwamba mtu anaweza kujipenda
na kujioa kwa kukosa wa kumuoa kwani cha muhimu ni mtu kujipenda kwanza kabla
ya kupendwa.
"watu
wengu huolewa bila ya kutafakari mara mbili kuhusu yule anayemuoa, '' Guess Jr
alisema.
Anadhani
kwamba pindi watu watakapomuona Eleby anavyojishughulikia mwenyewe, huenda
akapata ushindani.
"ni
mrembo, anafanya kazi kwa bidii na anasifika duniani na pia anaona uamuzi wake
umewapa gumzo watu wengi.
Chapisha Maoni