Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Na Mwandishi Maalumu, Dar es Salaam

DEREVA wa basi la UDA lenye namba za usajili T. 696 CVB ambalo liligonga treni juzi na kusababisha kifo cha mtu mmoja papo hapo na majeruhi zaidi ya 20, Majuto Hamis (PICHANI) amefunguka na kuzungumzia tukio hilo.

Akizungumza na matukionamaisha katika wodi 2B iliyoko kwenye jengo jipya la Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI) ambako amelazwa kwa ajili ya kupata matibabu, alisema ilikuwa ajali mbaya mno.

“Sikutegemea…ilikuwa ni usiku wa saa tatu nilikuwa nimepakia abiria wangu wapatao 40 tulikuwa tunatoka Kariakoo kunaelekea Mbagala lakini safari yetu iliishia pale eneo la Kamata na sasa nipo MOI nikiwa nimevunjika miguu yangu yote miwili.

“Jambo ambalo nakumbuka, katika eneo lile, hakuna kielelezo chochote kinachomtaarifu dereva kuwa mbele yake kuna reli inakatisha kwenye barabara hivyo aendeshe kwa uangalifu.

“Sasa mchana huwa ni rahisi kujua kama kuna treni inakatisha maana kunakuwa na nuru tofauti na usiku kwani huwa kuna giza,” alisema.

Hamis alisema kwa kuwa hakuna alama ya kiashirio kwenye eneo hilo, alijisahau kibinadamu na kwamba alishtuka tayari ajali imetokea.

“Sikukumbuka kabisa nikawa naendelea na safari ghafla tukawa tayari tumekutana na treni ile na kupata ajali,” alisema kwa masikitiko.

Alisema hadi sasa hajui iwapo kondakta wake alisalimika katika ajali hiyo ingawa amesikia wengi walijeruhiwa.

“Naiomba serikali hasa Kikosi cha Usalama Barabara waende katika eneo lile wakaweke kibao ili ajali nyingine zisiendelee kutokea, tena ingefaa zaidi katika maeneo ambako reli inakatisha barabara pawe na mageti wakati treni inakatisha wafunge kwa muda,” alisema.

Ofisa Uhusiano wa MOI, Patrick Mvungi alisema walimpokea Hamis na majeruhi wengine baada ya kupatiwa srufaa toka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).

“Tuliwapeleka moja kwa moja katika chumba cha dharura na sasa wanapatiwa matibabu wodini,” alisema.

Naye Ofisa Uhusiano wa MNH Neema Mwangomo alisema hadi kufikia jana tangu aAjali hiyo itokee walipokea majeruhi 49.

“Majeruhi 19 walitibiwa na kuruhusiwa, 22 walipelekwa MOI hivyo MNH tumebaki na wanane,” alisema.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement