Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
http://www.thecitizen.co.tz/image/view/-/3218060/medRes/1335991/-/48831hz/-/pic+cardiac+intitute.jpg 
Na Veronica Romwald, Dar es Salaam
 
TAASISI ya Tiba ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) inatarajia kufanya tena upasuaji mkubwa wa kihistoria kwa kuweka betri katika moyo wa mtu mzima ambao unashindwa kusukuma damu kwenye mishipa ipasavyo.

Akizungumza na matukionamaisha hospitalini hapo, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa JKCI, Peter Kisenge alisema upasuaji huo utakuwa ni wa mara ya kwanza kufanyika nchini.

“Kweli tumefanya upasuaji mara nyingi hapa JKCI, lakini hatujawahi kufanya upasuaji huu wa kuweka betri kwenye moyo wa mtu mzima ambao misuli yake imechoka na haiwezi tena kufunguka, kusukuma damu kwenye mishipa,” alisema.

Alisema utendaji kazi wa moyo huo upo chini ya kiwango cha asilimia 20 ndio maana mgonjwa huyo atamfanyia upasuaji huo ili betri hiyo iweze kumsaidia moyo wake kufanya kazi sawa sawa. http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/3156790/medRes/1254283/-/ifc8fc/-/Muhimbili+Photo.png
Jengo la JKCI 

“Tutakwenda kuweka kifaa hicho ambacho kitaalamu kinajulikana kama Pacemaker CRTD kwa mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 68 ambaye moyo wake umechoka na hivyo kushindwa kusukuma damu kwenda kwenye mishipa ili isafiri mwilini na yeye aweze kuishi,” alisema.

Alisema iwapo mambo yatakwenda kama yalivyopangwa na kwa neema za Mwenyezi Mungu wanatarajia upasuaji huo kufanyika Agosti 13, mwaka huu.

“JKCI tutafanya upausaji huo kwa kushirikiana na madaktari bingwa wa moyo kutoka nchini Kenya na tuna imani kuwa tutafanikiwa,” alisema.

Hivi karibuni, Taasisi hiyo iliweza kufanikisha upasuaji mwingine wa kwanza kwa kuweka betri katika moyo wa mtoto mwenye umri wa miaka sita.
 
Kwa mujibu wa madaktari wa JKCI, mtoto huyo, Happiness Josephati (pichani na mama yake) hakuzaliwa na betri ya asili ambayo Mwenyezi Mungu huiweka katika kila mwili wa mwanadamu wakati ambapo viungo huumbwa akiwa tumboni mwa mama yake.

Elitruda Malley ambaye ni mama mzazi wa Happiness aliliambia gazeti hili kuwa awali alikuwa hawezi kufanya mambo ambayo watoto wa umri wake wanayafanya kwani kila mara alikuwa akipoteza fahamu.
Mkurugenzi wa jkci, Profesa Mohamed Janabi

Hata hivyo baada ya kufanyiwa upasuaji huo hivi sasa afya yake imeimarika na wakati wowote wataruhusiwa kurejea nyumbani kwao Arusha.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement