Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/3156790/highRes/1253303/-/maxw/600/-/ue3os8/-/Muhimbili+Photo.png 
Jengo la JKCI lililoko ndani ya Muhimbili

Na Mwandishi Maalumu, Dar es Salaam

ASKARI wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wamechangia damu katika Taasisi ya Tiba ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) ikiwa ni hatua ya kuwezesha upasuaji wa watoto wapatao 70 wanaosubiri upasuaji huo.
 http://mtanzania.co.tz/wp-content/uploads/2016/05/Profesa-Mohamed-Janabi-247x300.jpg
Akizungumza na mtandao huu hii leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Profesa Mohamed Janabi (pichani) amesema wamepata chupa zaidi ya 20.

“Tunashukuru kwa askari wetu wa JWTZ kuchangia damu, tuna watoto zaidi ya 70 wanaosubiri kuanza kufanyiwa upasuaji kuanzia Agosti 9 hadi 19, mwaka huu.

“Lakini wakati huo huo tunakabiliwa na uhaba wa damu, tumepata chupa zipatazo 24 toka kwa wanajeshi wetu na kesho wamesema watakuja tena, tunaomba watanzania wengine nao waungane nao kuja kuchangia damu ili tuokoe maisha ya watoto hawa,” amesema.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiELfZTG4Uck86D8p9PyQoWlHwtBsULqE8_lpi3SzoFdeIYWlht4UcQgAZ8okzO_CI_Txn7RmnGSuUUmOwJVw3QCsn9Tb_whSR_vln0F1xjAKGm9PfltNtcMIZF6MJHNvubUnRfL9yN_cMO/s1600/002.JPG Msemaji wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ),Kanali Ngemela Lubinga(aliyesimama) alipokabidhi taarifa kwa mkuu wa mkoa Paul Makonda juu ya maadhimisho ya miaka 52 ya JWTZ ambapo pia alisema watajitolea kuchangia damu.

Amesema JKCI wanatarajia kuwafanyia upasuaji huo kwa kwa kushirikiana na wataalamu wenzao wa nchini Marekani na Italia.
“Kuna watoto wapatao 500 wanasubiri huduma ya upasuaji. 

Tunaanza na hawa 70 Agosti 9 hadi 19, mwaka huu, tutatumia njia ya upasuaji pasipo kufungua kifua ambapo  kwa siku tutaweza kuwafanyia watoto 11 hadi 12,” amesema.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement