Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEibFqP6o8o9K2YCsZdWzuahmzBOESsiCac92JR45uVHhyeV0Pox76cEwWOse36qqlzUq-kubS5GMMWff7eGh1-lkuE-eKLozNvnOHcA3UAp6yOT5Q3wCXCZh3Y1ED27pTxElA6ElmhoslI/s400/new-jenerali-ulimwengu1.jpg 
MWANAHABARI nguli nchini Jenerali Ulimwengu ambaye alilazwa katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI) kwa matibabu ameruhusiwa.

Akizungumza na mtandao huu juzi katika wodi namba H saa chache kabla ya kutoka kurejea nyumbani kwake, Ulimwengu alisema anamshukuru Mungu afya yake imeimarika.

"Jambo ninalokumbuka … siku ile nilikuwa nimetoka kuwasalimia ndugu zangu, sijui nini kilitokea nikapatwa na ajali iliyonifanya nilazwe hapa MOI,” alisema.
 Image result for AJALI YA ULIMWENGU
Ulimwengu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wahariri wa gazeti la Raia Mwema alipata ajali ya gari usiku wa Agosti 25, mwaka huu.

Alipata majeraha katika sehemu mbalimbali za mwili wake hali ambayo ilipelekea kulazwa hospitalini hapo ili kupata matibabu.

Kwa mujibu wa Ofisa Uhusiano wa MOI, Patrick Mvungi ajali hiyo inadaiwa kuwa ilitokea kati ya makutano ya barabara ya Ally Hassan Mwinyi na Kenyata.

Mvungi alisema Ulimwengu ameruhusiwa kurejea nyumbani baada ya daktari wake kuridhishwa na maendeleo ya afya yake.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement