Na Mwandishi Makini, Dar es Salaam
MCHUNGAJI Kiongozi wa Kanisa la Mlima wa Moto, Mikocheni B Assemblise of God, Dk. Getrude Rwakatale amesema sadaka zitakazokusanywa kanisani hapo jumapili ya wiki hii zitakwenda kuwalipia faini wafungwa walioko gerezani waliotimiza vigezo lakini wameshindwa kulipa kwa kukosa fedha na hivyo kutupwa magerezani.
Mchungaji Rwakatale ametamka ahadi hiyo juzi mbele ya Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole, Augustino Mrema saa chache baada ya kumpongeza na kumteua kuwa msimamizi wa harambee ya kukusanya fedha za kuwalipia wafungwa waliokidhi masharti ya Parole.
Awali akizungumza Mrema alisema kukosekana kwa fedha ya kukamilisha mchakato wa sheria ya Parole kwa
wafungwa mbalimbali nchini waliomaliza nusu ya kifungo chao gerezani ni
miongoni mwa sababu yakuwepo mrundakano wa wafungwa katika magereza
Tanzania.
“Ni lazima maofisa wa parole wafuatilie nakala ya hukumu kwenye
mahakama iliyomukuhumu na waende kuonana na uongozi wa kijiji au mtaa
ambapo mfungwa atenda kuishi anapotoka gerezani ikiwa ni pamoja na
kuonana na familia yake na pia kuonana na watu waliowakosea ili jamii ya
eneo hilo itambue kuwa ataachiwa huru” amesema
Aidha, Mrema
amewataka maofisa wa parole kote nchini kuwatembelea wafungwa waliopata
Parole ili wafungwa wengi wenye sifa za kutolewa kwa sheria ya Parole
wasiendelee kuteseka magerezani bali waende kuungana na familia zao
sambamba na kuongeza nguvu kazi.
Kutokana na kutotengwa fedha
kwa ajili ya kushugulikia suala hilo, Mwenyekiti huyo wa Parole Taifa,
amemteua Mama Getrude Lwakatare kuwa mratibu wa kuchangisha fedha kwa
kushirikisha viongozi wote wa dini nchini kushiriki harambee kwaajili ya
kuchangisha fedha za kuwatoa wafungwa magerezani na kupunguza
msongamano katika magereza nchini.
“Napendekeza kufanyike
harambee kwenye makanisa yote nchini, siku ya Jumapili moja ili sadaka
zote zikatumike kuwalipia faini wafungwa waliopo magerezani” amesema
Mrema amesisitiza kuwa wanaolengwa na Parole siyo wanye makosa ya ubakaji, mauaji, wizi kwa kutumia silaha na makosa mengine.
Naye Mchungaji Lakatare amewataka watanzania kuangalia
taifa kwanza kwani kina baba wengi wenye nguvu watarudi katika jamii na
kusaidia katika uzalishaji mali sambamba na kutatua matatizo ya kiuchumi
na kimaendeleo katika familia zao.
“Tutaunganisha familia zilizo
sambaratika na kutaabika baada ya mzazi mmoja kufungwa miaka 6 pengine
kwa kukosa faini ya milioni moja tuu, tutaondoa msongamano wa wafungwa
na kulinda afya zao kutokana na magonjwa wanayopata wakiwa gerezani”
amesema
Mchungaji Lwakatare amesema anaunga mkono
jitihada za bodi ya Parole Taifa na siyo kuwalinda waalifu kama ambavyo
wengine watatafsiri kwani kurejesha familia ni miongoni mwa kustawisha
jamii huku akinukuu maneno ya kidini yanayolenga kuwakomboa walioko
kwenye vifungo na taabu mbalimbali ndani ya jamii.
Chapisha Maoni