Hiyo ni baada ya Hospitali ya Taifa Muhimbili hii leo kupokea msaada wa luninga yenye ukubwa wa inchi 50 na king’amuzi chake wenye jumla ya Sh milioni 2.4 toka kwa Umoja Mahiri wa Kibosho (UVIKI). Luninga hiyo itafungwa katika wodi namba mbili ya wazazi maarufu wodi ya Magufuli ambapo itatumika kutoa elimu ya afya na lishe kwa wale wanaofika kliniki.
Fungua tuone kilichomo ndani yake.
Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, Mwenyekiti wa
Umoja huo, Marcel Mushi alivishauri vikundi vingine kuiga mfano toka kwao na
kuisaidia jamii.
Waaao
Shukrani zikaanza kumiminika .
“Huu kwetu ni mwanzo, tumetoa luninga na king’amuzi chake
vile vile tunachangia damu chupa 40 kwa ajili ya kusaidia wenye uhitaji,”
alisema.
Naye Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma na Huduma kwa
Wateja, Aminiel Aligaesha alisema kupitia lungina hiyo sasa wataanza kutoa
elimu ya afya kidigitali kwa wanawake watakaokuwa wakifika kupata huduma za
kliniki.
“Wametupatia na dvd player yake, tutarekodi vipindi vya afya,
kuna masomo mengi ya lishe tutakuwa tunayaonesha wakina mama wanaokuja kliniki
kila siku ili waelimike,” amesema.
Chapisha Maoni