Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


https://i.ytimg.com/vi/6KfuMh5d810/hqdefault.jpgNA VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM

IDADI kubwa ya watoto wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 18 hasa wa kike wanafanyiwa vitendo vya ngono katika ngoma za usiku ‘vigodoro’.

Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto wa Wizara hiyo, Sihaba Nkinga alisema hayo juzi alipozungumza na MTANZANIA, saa chache baada ya kumalizika kwa semina ya siku moja ya waandishi wa habari kuhusu masuala ya ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto.

Nkinga alisema watoto wengi waliohojiwa na maofisa wa Wizara hiyo walikiri kufanyiwa vitendo hivyo kwenye vigodoro hali iliyowapelekea wengine kupata ujauzito wakiwa na umri mdogo.

“Hali ya ukatili wa kijinsia nchini ni mbaya, wanawake wengi na watoto wanafanyiuwa ukatili, lakini mwaka 2009 tulifanya utafiti na matokeo hayo yalitoka mwaka 2011, watoto wengi waliohojiwa walikiri kufanyiwa vitendo vya ngono kwenye vigodoro.

“Tuligundua pia zipo baadhi ya mila na desturi ambazo watu wamezishikilia ambazo ni kikwazo katika mapambano dhidi ya mimba na ndoa za utotoni, kuna familia nyingine zina umaskini ambao nao unachochea tatizo kwani familia zinaona watoto wa kike kama kitega uchumi chao,” alisema.
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj0ZzrSBdMET3N5wZ5E76PtVy_KXGgNVQkxF91hBZ9Adg3ksr2gNIJrGOG8SIP7z2LveQNI-0S703MAcyyRRYmGysqtmnVRQKsY-A_auOA332wT5cZcoiAKj71kj-gu-bSZ9VsT0OEjKJZ2/s640/DSC_0433.JPG
Nkinga (pichani) alisema kutokana na hali hiyo jamii bado inahitaji elimu zaidi ili kupambana na ongezeko la idadi ya ndoa na mimba za utotoni na vitendo vya ukatili wa kijinsia.

“Leo hii tunalalamika kuna mmonyoko wa maadili lakini kiukweli suala hilo ni matokeo ya ukatili ambao wengi walifanyiwa wakati wa utotoni.

“Takwimu zinaonesha kuwa watoto wanafanyiwa vitendo vya kikatili lakini jamii haifuatilii, kwa mfano utafiti wa mwaka 2010 unaonesha asilimia 39 ya wanawake wenye umri wa miaka 15 hadi 30 wanafanyiwa ukatili.

“Na kati ya watoto saba, mmoja anakuwa amefanyiwa ukatili, hivyo tunahitaji ushirikiano wa karibu wa kila mmoja kufikisha ujumbe kwa mwenzake kwamba hali ni mbaya,” alisema.
 
Naye Magreth Musai (mwenye MIC) alisema serikali iliona suala hilo kuwa ni changamoto na kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo wakiwamo UNICEF kutengeneza mpango kazi wa kitaifa wa kukabiliana na ukatili wa kijinsia wa miaka mitano.

“Awali kulikuwa na mipango nane ambayo tumeipitia kwa pamoja na kutengeneza mpango mmoja na lengo ni kutokomeza ndoa na mimba za utotoni na ukatili wa kijinsia, tutauzindua wakati wowote kuanzia sasa,” alisema.

Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Wanawake (UNWOMEN), Maria Karadenizli akizungumza na waandishi wa habari kuhusu vitendo vya ukatili wa kijinsia pamoja na kuomba ushirikiano wa serikali pamoja na vyombo vya habari ili kutengeneza mpango mkakati wa kuondoa vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto.

Usia Nkhoma Ledama kutoka UNICEF akieleza jambo wakati wa semina kwa waandishi wa habari iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Wanawake (UNWOMEN) na kuwakutanisha wadau mbalimbali wa serikali na kijamii iliyofanyika katika Hoteli ya Double Tree jijini Dar Es Salaam

Pedro Guerra kutoka UNICEF akizungumza jambo katika semina iliyowahusisha waandishi wa habari ili kuweza kuripoti habari za kijinsia hasa za ukatili wa mama na mtoto.

Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Wanawake (UN WOMEN) Lucy Tesha akizungumza jinsi shirika hilo lilivyoweza kupambana na unyanyasaji wa kijinsia kwa mtoto wa kike
Baadhi ya waandishi wa habari wakichangia mada inayohusu ukatili wa mama na mtoto katika semina iliyofanyika katika hoteli ya Double Tree jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa kwenye semina.
Ruth Ayisi kutoka UNICEF  akitoa ufafanuzi kuhusu njia  wanazoweza kuzitumia waandishi wa habari kuripoti habari za unyanyasaji wa kijinsia kwa mama na mtoto.Baadhi ya waandishi wakijadiliana

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement