TENKI la kuhifadhia majitaka katika Soko la Kimataifa la Samaki
(Feri), limepasuka na hivyo kukabiliwa na changamoto za kulipuka kwa
magonjwa ya mlipuko.
Mwenyekiti wa Soko hilo, Omary Mtolea,
amesema tatizo la miundombinu ni changamoto inayolikabili soko hilo kwa
muda mrefu.
Mtolea amesema jambo hilo limesababisha chemba moja kupasuka na kumwaga maji hayo machafu nje ya utaratibu.
Amesema baada ya kuona tatizo linazidi kuwa kubwa waliamua kupeleka
malalamiko yao Halmashauri ya Ilala ambao waliahidi kulitengeneza,
lakini hadi sasa hawajaona jitihada zozote kunusuru afya za wadau wa
soko hilo.
“Mkandarasi anayesimamia usafi na ushuru katika soko hilo, anatarajia kumaliza mkataba wake ifikapo Desemba mwaka huu.
“Hivyo tutajipanga upya jinsi tutakavyoona inafaa ikiwa ni pamoja na
kufanya tathimini kuweza kujiridhisha kama anaweza kuendelea au kuachia
ngazi,”amesema Mtolea.
Chanzo: MTANZANIA
Chapisha Maoni