Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/3489584/highRes/1514591/-/maxw/600/-/bu1xx8/-/pic+siri+nzito+maiti.jpgNA VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM

VITENDO vya mauaji kisha miili kutiwa kwenye viroba na kwenda kutupwa ama mtoni au kutelekezwa mahali popote vimeibuka nchini.

Desemba 6, mwaka huu kuliripotiwa tukio la aina hiyo, huko katika mkoa wa Pwani eneo la Bagamoyo katika mto Ruvu.

Katika eneo hilo wananchi walihisi uwepo wa harufu kali kabla ya kuona viroba vikiwa vinaelea juu ya maji ambavyo walivitilia shaka.
 http://www.ippmedia.com/media/picture/large/MwigulluNcemba.jpg
Waziri wa Mambo ya Ndani Mwigulu Nchemba

Wakazi hao wali baada ya kugundua miili hiyo ikielea katika Mto Ruvu, walimpigia simu Mwenyekiti wao wa Kitongoji cha Mtoni, Maneno Mafumba ambaye alifika kujionea tukio hilo.

Mwenyekiti huyo alifika hapo akiwa ameongozana na Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Bagamoyo, OCD Maro wakiwa wameambatana pia na madaktari wa Hospitali ya Bagamoyo.

OCD huyo aliamuru miili hiyo kuopolewa lakini haikuchunguzwa kwa madai kuwa ilikuwa imeharibika vibaya na hivyo ikaamuriwa izikwe, jambo ambalo lilitushangaza wengi na kutuacha na maswali.

Kwamba kwanini haikuchunguzwa kujua kama watu hao waliuwawa kwa sumu au la maana wengi wanahisi kuwa huenda waliuwawa kwa njia hiyo, tunashukuru ilifukuliwa kwa ajili ya uchunguzi ingawa bado miili hiyo haijtambulika hadi sasa.

Zikiwa zimepita siku chache tu tangu kutokea kwa tukio hilo, mwili mwingine umekutwa tena ukiwa umefungwa kwenye kiroba na kutelekezwa katika eneo moja huko mkoani Kilimanjaro.

Kwa kuwa wananchi tulipaza sauti kuhoji sababu za kutochunguzwa kwa vifo vya watu wale saba ambao Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba alisikika akisema kwamba huenda ni ya wahamiaji haramu.

Tumeshuhudia awamu hii mwili uliokutwa huko Kilimanjaro ukiwa umechukuliwa kwenda kufanyiwa vipimo kabla ya kuzikwa.

Si lengo la makala haya kuhoji kauli ya Waziri Mwigulu jambo ninalotaka kueleza hapa ni kuhusiana na mauaji haya yalioanza kutokea hapa nchini.

Nia yangu ni kuvihimiza vyombo vya dola kutokufumbia macho vitendo hivi kusudi visije vikashamiri katika nchi yetu.

Kwamba tusiishie kusema wale walikuwa wahamiaji haramu kasha tukakaa kimya pasipo kuchukua hatua za ziada za kuimarisha mifumo yetu ya ndani.

Hapa vyombo vya dola visiachwe vifanye kazi peke yake, jamii inapaswa pia kushirikishwa.

Wakati fulani nilipata kusoma makala ya mwandishi mmoja ambaye ni mkongwe kidogo katika fani.

Mwandishi huyo alikuwa akieleza juu ya mfumo wa nyumba kumi ulivyokuwa ukifanya kazi na ambavyo ulisaidia kuimarisha ulinzi wan chi kuanzia huko majumbani.

Leo hii utaona jinsi ambavyo tunashindwa kuimarisha ulinzi wetu kwa sababu hata huko mitaani wengi hatujuani.

Utamkamata nani umwambie kuwa ni mhamiaji haramu hata hao wajumbe wa nyumba kumi baadhi yao hawawajui watu wanaoishi kwenye mitaa yao.

Hakuna utaratibu mzuri wa kuwatambua, ingawa kwa mkoa wa Dar es Salaam kwa mfano nilipata kumsikia mkuu wa mkoa Paul Makonda akiwaagiza kuhesabu watu wanaoishi katika kila nyumba.

Lakini katika eneo ninaloishi binafsi sijaona jambo hilo likitekelezwa, sijui kama maeneo mengine viongozi walitii agizo hilo.

Ni wakati wa kuamka na kufanya ufuatiliaji kusudi iwe rahisi kubaini mambo kabla matukio hayajatokea katika nchi yetu.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement