NA SHUSHUSHU WETU
WATANZANIA tuna kila sababu ya kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumjalia dada yetu huyu mwenye sauti ya kumtoa nyoka pangoni kurejea tena katika hali yake ya kawaida.
Itakumbukwa kwamba alitumbukia kwenye dimbwi la dawa za kulevya ambapo alipambana mno kujinasua tangu alipookolewa na Rais wa Awamu ya Nne, Dk. Jakaya Kikwete.
Naam sasa anaendelea kusonga mbele baada ya kupata msaada na Wiki hii amepiga picha zake akiwa katika muonekano mpya kabisa.
Katika picha hizo Ray C amevalia na kutokeleza katika muonekano wa kihindi huku akivutia.
Chapisha Maoni