RAIS Dk. John
Magufuli, ametoa zawadi ya vyakulakwa watu walio katika
makundi maalum wakiwemo watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi,watu
wenye ulemavu pamoja na wazee.
Zawadi hizo zimekabidhiwa kwa wasimamizi wa vituo saba Dar es Salaam na Kamishina Msaidizi, Ustawi wa Jamii wa Wizara ya Afya
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Beatrice Fungamo kwa niaba ya Rais Magufuli. Amesema Rais Magufuli ametoa zawadi ya mbuzi na mafuta ya kupikia zenye thamani ya Sh milioni 8.475.
Amesema Rais Magufuli ameyakabidhi makundi hayo zawadi hizo kwa ajili ya kuwawezesha kusherehekea sikukuu ya Krismasi na Mwaka mpya kama makundi mengine.
Chapisha Maoni