RAIS
wa Tanzania Dk. John Magufuli na Mkewe Mama Janeth Magufuli
wamemtembelea na kumpa pole Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es
Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.
Hatua
hiyo ni kufuatia kifo cha Dada yake aitwaye Efrazia Pengo aliyefariki
dunia jana tarehe 22 Desemba, 2016 katika Kijiji cha Mwazye, Wilaya ya
Sumbawanga Mkoani Rukwa akiwa na umri wa miaka 79.
Chapisha Maoni