NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM
Mpigapicha maarufu Mpoki Bukuku amefariki dunia leo katika Taasisi ya Mifupa (MOI), alikokuwa amelazwa akipatiwa matibabu.
Taarifa za kifo chake zimethibitishwa na Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano kwa Umma (MOI) Almas Jumaa.
"Ni
kweli Mpoki amefariki dunia mchana huu, alipokelewa jana usiku baada ya
kupata ajali ya gari maeneo la Mwenge ITV, taarifa zaidi tutazitoa
baadaye," alisema Almas.
Taarifa zinasema marehemu alikuwa
ametoka kazini jana usiku, akagongwa na gari maeneo ya Mwenge na
kuvunjika miguu yote miwili na mkono mmoja.
Mpoki
Bukuku amewahi kufanya kazi kama Mpiga Picha Mkuu katika gazeti la
Mwananchi, linalochapisha magazeti ya Mwananchi, The Citizen na
Mwanaspoti. Pia amewahi kufanya kazi magazeti kadhaa likiwemo Majira na
Nipashe.
Blog ya matukionamaisha inatoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na marafiki,
Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.
Amen.
Chapisha Maoni