Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
NA CATHERINE SUNGURA, WIZARA
 
WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu ametembelea kituo cha Afya cha Gairo na kukabidhi mabati 100 kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).
 
Fedha hizo ni kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya wazazi katika kituo hicho. 
 
Hii ni kufuatia ahadi yake aliyoitoa Julai, mwaka huu alipofanya ziara ya kikazi wilayani Gairo kukagua utoaji wa huduma za Afya.

Akikabidhi mabati hayo jana Waziri Ummy alisema kipaumbele chake cha kwanza ni afya ya mama na mtoto" hivyo atahakikisha huduma kwa mama wajawazito na watoto zinaimarika katika vituo vya kutolea huduma za afya vya umma kote nchini. 

Hivyo aliitaka Halmashauri ya Wilaya ya Gairo kusimamia vyema utoaji wa huduma ya afya ya uzazi na mtoto kwani kufanya hivyo kutatatua takribani asilimia 70 ya changamoto za afya nchini. 

Aliiagiza halmashauri itumie vyanzo vyake vya mapato vya ndani kununua baadhi ya vifaa tiba kama x - ray na ultra - sound ili kuboresha huduma za uchunguzi wa wagonjwa.

Waziri Ummy pia aliuelekeza uongozi wa  Halmashauri ya Wilaya ya Gairo kuhakikisha inaunda kamati za afya za vituo na wahakikishe zinatekeleza majukumu yake ipasavyo ikiwemo matumizi mazuri ya dawa. 

"Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dr John Pombe Magufuli imetoa kipaumbele kwa sekta ya afya hususani upatikanaji wa dawa kwenye vituo vya afya," alisema.

Akitoa mfano wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo alisema, mwaka wa fedha wa 2015/16 walitengewa kiasi cha shilingi milioni 89 lakini mwaka huu wa fedha wa 2016/17 bajeti ya dawa imeongezeka hadi kufikia milioni 198 na hadi sasa wameshapatiwa shilingi milioni 115. 

Aliwataka viongozi wa Halmashauri hiyo kusimamia vizuri matumizi ya fedha hizo ili  tuweze kuwa na dawa za kutosha katika vituo vya afya.

Aliwataka pia viongozi hao wasimamie na wahamasishe wananchi wajiunge na mfuko wa afya ya Jamii - CHF, ambapo kimsingi bima hii inawasaidia sana wananchi kupata huduma za afya pindi wanapohitaji kupata huduma za matibabu hususani wanapokuwa hawana fedha taslimu. 

"Wananchi wengi wamekuwa wakishindwa kumudu gharama za matibabu kutokana ukweli kwamba gharama za matibabu zinaongezeka kila siku. Hakikisheni pia mnawatambua wazee wote wasiojiweza na kuwapatia vitambulisho ili viwasaidie wakati wanapohitaji kupata huduma ikiwemo huduma za afya," aliwahimiza.

Hata hivyo, alipongeza ubunifu uliofanywa na uongozi wa mkoa wa Morogoro kwa kuanzisha mfumo ujulikanao kama JAZIA, utaratibu huo unatumika kuhakikisha dawa zote zinakosekana kupitia Bohari ya Dawa, zinanunuliwa kupitia vyanzo vingine vya mapato ili kuhakikisha zote muhimu zinapatikana kwenye vituo vya matibabu.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement