Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


 http://mobile.mwananchi.co.tz/image/view/-/2039710/medRes/604714/-/13vt9vo/-/dawadawa.jpg?format=xhtml

Vijana wakijidunga dawa za kulevya

NA VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM

KUNA wimbi la wasanii nchini kutumbukia katika matumizi ya dawa za kulevya za aina mbalimbali na upo mjadala kwanini wamekumbwa na ‘pepo’ hilo.

Wengi wanahoji sababu zinazowafanya wasanii kuingia katika mkumbo huo licha ya kuwa wana uwezo wa kutumia vipaji vyao kujipatia fedha halali.

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Akili,Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dk. Cassian Nyandindi ametaja sababu kuu inayochangia kundi hilo kuingia katika janga hilo.
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj6c8L0GD3OhDOYC-2nuvGoFxlDro3PbNHA-c0QxM7UnoHiSvtxnx32NqUIPbI5TBY6uU0AkgcQM29jPj_jWT-cKmxXpOmdsZCTx-I1M5ZeGdSlC1HGysGWNvv-bg05AV7Mk6ZPDRN3buw/s1600/MUHIMBILI.png
Akizungumza na matukionamaisha hivi karibuni jijini Dar es Salaam, Dk. Nyandindi alisema wengi hufanya hivyo kwa kigezo cha kuondoa aibu usoni eti wakati wanapokuwa wakitumbuiza jukwaani.

“Kuna sababu nyingi zinazochangia mtu kutumbukia katika matumizi haya, wapo ambao hupata vishawishi toka kwa ndugu, marafiki zao wa karibu, kuna ambao hutumbukia kutokana na kupata matatizo ya kisaikolojia, wengine hutumia ili kukidhi haja zao na malezi mabovu.

“Lakini kwa hawa wenzetu wasanii wengi wanadhani kwamba anapotumia dawa za kulevya uwasaidia kuondoa aibu ili waweze kufanya vema pindi wanapopanda jukwaani,” alisema.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiomUpxJt_evsESXVtcUPLe8tJgCGWZjVnr8wOm919GQmPDIcMx61HqDDLNNnQI3NMV4pM2air7tkKdmCO1DwG_b8uLbi6HrECmucuEoxAPPmjX9pRUpPh_jBMxe3CfH2htLWemmtASuN7x/s640/madawa.jpg
Daktari huyo alisema awali mtumiaji huona kuna manufaa pasipo kujua kuna hatari kubwa mbele yake.

“Wapo ambao hujikuta wakitumia dawa kupita kiasi jambo ambalo hufanya wapoteze fahamu au hata kupoteza maisha,” alisema.
 
Aliongeza “Mtu aliyezidisha kiwango cha dawa utaona analala sana, anasinzia kila mara, anakoroma, mapigo yake ya moyo yanakuwa chini kuliko kawaida, uwezo wake wa kupumua (breathing rate) unashuka chini, kwa kawaida huwa dakika 16 hadi 20 lakini hawa hufikia hadi dakika chini ya 12, ni hatari, pia muda mwingi huonekana wakiwa wamening’iniza kichwa chini (head bending),” alisema.

Alisema watu wanaotumia dawa za kulevya huanza kuonesha dalili ambazo kitaalamu zinaitwa ‘with draw features’ wenyewe (watumiaji) wanaita alosto.
 https://blogger.googleusercontent.com/img/proxy/AVvXsEiAGw5Z2KUj-S6ySnJVfivVfNa5dKvR_1yYC6QRKWG61EcCH3y-Y_mgVhJjBsqo0iMpUB8ingOmsLKGX87vGUaqX4dvQAqUgylGpaVNlb-TZM83yMJkgpLxbiV7UywwplL30YpjOk2XqKecXFoysbHmXq0VfHNXik8D5f3qDO7bPZBac3i3WzQpOAzJLvCQoDq_6tJKFUHdG30GxXbs3-Me5_C4I4Y45pVpuKfCo0hDAMODNrkJ2CzB6koUlFnsdP4GMA=w5000-h5000Dawa za kulevya zilizowahi kukamatwa na Jeshi la Polisi Tanzania
“Hasa pale anapokosa dawa anapata maumivu ya mwili yaliyopitiliza, maumivu ya tumbo, kuharisha, kutetemeka, kutokwa na jasho jingi, kamasi, machozi na kukosa usingizi ni miongoni mwa athari zinazowapata watumiaji wa dawa za kulevya,” alisema.

Alisema kiujumla matumizi ya dawa za kulevya yanaathiri mfumo wa ubongo.

“Hadi sasa kuna takribani watu 3,500 ambao ni waathirika wa dawa za kulevya wanaopatiwa huduma ya methadone katika vituo vinne vilivyofunguliwa nchini.

“Kituo cha Muhimbili kilikuwa cha kwanza kufunguliwa mwaka Februari 2011, Novemba 2012 kikafunguliwa cha Mwananyamala, Machi 2014 Temeke na Zanzibar 2015,” alisema.

Daktari huyo alisema kwa mujibu wa ripoti ya mwaka 2014 ya Tume ya Taifa ya Kudhibiti Dawa za Kulevya (NACP) inakadiriwa kuwa watu 550,000 nchini wanatumia dawa ya kulevya ya heroin.

“Kati ya watumiaji hao, 50,000 hujidunga sindano na kati ya idadi hiyo asilimia 50 wanaishi katika jiji la Dar es Salaam, katika jiji hilo Wilaya ya Kinondoni inaongoza kwa kuwa na watumiaji wengi wa dawa za kulevya,” alisema.

Dk. Nyandindi alisema ripoti hiyo inaeleza mikoa mingine iliyo na idadi kubwa ya waathirika wa dawa za kulevya ni Arusha, Tanga, Kilimanjaro, Dodoma, Mbeya, Pwani, Mwanza na Morogoro.

Alisema kwa kuwa wengi hujidunga sindano inachochea kuongezeka kwa kasi ya maambukizi ya virusi vya ukimwi.
“Kwa mujibu wa ripoti hiyo ya (NACP), kiwango cha maambukizi ya VVU kwa kundi hili ni asilimia 20 hadi 50 wakati kwa kundi la jumla (general population) ni asilimia 5.1 hii ni kwa sababu wakishajidunga sindano hushindwa kufanya maamuzi sahihi na kujikuta wakifanya ngono zembe,” alisema.

Aliongeza “Matumizi ya dawa za kulevya uchochea pia mtu kupata homa ya ini (Hepatit B na C) na kwamba kiwango cha maambukizi ya kifua kikuu ni kikubwa kwa kundi hilo.

“Lakini siku hizi kwa kuwa uingizwaji wa dawa umezibitiwa wapo ambao wanaona watumie njia mbadala ya kupunguza alosto kwa kunywa ama pombe kali au dawa za usingizi jambo ambalo linaongeza tatizo,” alisema.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement