NA MWANDISHI WETU, KILIMANJARO
KATIKA kile kinachoonekana kuwa na uhakika na kauli yake, Mbunge wa
Rombo, Joseph Selasini (Chadema) amesema atajiuzulu ubunge wake kama
mradi wa maji wa Chigongwe utatoa maji katika siku 21 zijazo.
Nadhiri hiyo imetokana na ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) katika miradi kadha ya Manispaa ya
Dodoma ukiwemo wa Chigongwe ambao ulionekana kujawa na madudu kibao.
Selasini amesema, mazingira yaliyopo katika mradi huo yanapingana na
kauli ya Kaimu Mhandisi wa Maji wa Manispaa ya Dodoma, Majuto Eliufoo
ambaye aliomba kamati hiyo kumpa wiki mbili ili maji yaanze kutoka.
Mbunge huyo pamoja na kusema hayo, pia aliungana na wabunge na
Mkurugenzi wa Manispaa ambao wamesema wazi kwamba haiwezekani katika
wiki mbili maji yatoke na yeye (Eliufoo) kung`ang`ania kuwa itawezekana.
“Mheshimiwa Mwenyekiti, tuwe wakweli kwenye mambo ya msingi, na mimi
nataka kuweka ukweli kwenye kumbukumbu kwamba, mradi huu ukianza kufanya
kazi ndani ya wiki tatu tangu leo lazima na nisisitize kuwa itakuwa
lazima kwa mimi kujiuzulu nafasi yangu ya ubunge,” amesema Selasini.
Mbunge huyo amesema anazo taarifa kuwa mradi huo wa maji katika eneo
hilo ulianzishwa kisiasa ndiyo maana wataalamu hawajui chochote.
Mhandisi Eliufoo amesema, mradi huo una thamani ya Sh milioni 533 na
tayari mkandarasi Kampuni ya Buyungu General Enterprises imeshalipwa
kiasi cha Sh milioni 409 huku akisema kazi katika mradi imemalizika kwa
asilimia 95.
Chanzo: Habari Leo
Chapisha Maoni