Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgGxi4l5-rEort3Gq_lSm6mnpLy2S-LwTGKQxqbtyXm8eXs1qxQrV_UzdZfmYkLFcx2cRK-IB6pCR3gxLGL1chwx19HQdUL4zIGxoS8MBMLFDWNgwlAUoeE2g2eYRgynuIuHqdv_-jXHlJg/s1600/9.jpgNa Veronica Romwald, Dar es Salaam

TAASISI ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI) inatarajia kufanya kampeni maalumu ndani ya mwaka huu ya kuhamasisha jamii kutambua jinsi ya kuepuka mama kuzaa mtoto mwenye tatizo la kichwa kikubwa na mgongo wazi.

Mkurugenzi wa Tiba wa MOI, Dk. Samwel Swai ameeleza hayo mapema leo alipozungumza na waandishi wa habari walipotembelewa na viongozi wa dhehebu la Shia ambao wameahidi kusaidia matibabu ya watoto 40 yaatakayogharimu Sh milioni sita.

“Tatizo hili lipo kwa muda mrefu sasa nchini, leo idadi imeongezeka kwa sababu jamii imepata uelewa, tunajitahidi kuwatibu kwa kadri ya uwezo wetu, tiba yao ni mtambuka na ina vitu vingi mno kuikamilisha, tunahitaji damu ya kutosha, usafiri wa kuwatoa huko walipo, dawa za usingizi na vifaa vya kutosha ili kuwahudumia,” amesema.

Dk. Swai (anayezungumza) amesema wamejitayarisha kuwasaidia wale waliowaandaa huku lengo lao kwa sasa ikiwa ni kutoa elimu kwa wananchi.

“Ni tatizo linaweza kuzuilika kwa kutumia lishe (folic acid) ambayo hupatikana kwenye baadhi ya vyakula lakini tunatoa vidonge maalumu vya folic acid, mama anatakiwa ameze miezi mitatu kabla ya kubeba ujauzito,” amesema.

Amesema pia wamekusudia kupata wodi maalumu na wataalamu watakaoshughulika kuwasaidia watoto hao peke yao.

“Tukihamia rasmi huku jengo jipya kule kwenye jengo la zamani tutaweka chumba kimoja cha upasuaji maalumu kwa ajili ya watoto hawa peke yao,” ameweka wazi.

Amesema jumamosi hii wanatarajia kuwafanyia upasuaji kati ya watoto 25 hadi 30 ambao tayari wameandaliwa.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement