Na Catherine Sungura, W. Afya
WADAU mbalimbali wa sekta ya Afya wametakiwa kufanya juhudi katika
kuimarisha afya ya mama mjamzito na mtoto nchini ili kupunguza idadi ya
vifo na kujenga taifa imara.
Hayo yamesemwa jana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee
na Watoto Mh. Ummy Mwalimu wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 24 wa
Wanasayansi wa ( AGOTA) uliofanyika jijini Dar es salaam .
Waziri ummy amesisitiza kuwa vifo kwa wanawake wenye ujauzito bado ni
tatizo sugu nchini, ambalo linahitaji jitihada na nguvu zaidi kupambana
nalo ili kutokomeza kabisa tatizo hilo Tanzania.
“Naishukuru taasisi ya AGOTA kwa jitihada inazofanya ikiwemo
kuhamasisha uzazi wa mpango,kufanya tafiti mbali mbali, kushauri na
utoaji huduma ya Afya kwa mwanamke” alisema Waziri Ummy.
Kwa upande wake Rais wa AGOTA Prof. Andrea Barnaba Pembe ametoa
pongezi kwa Waziri Ummy Mwalimu kutokana na jitihada anazoendelea
kufanya kupitia Serikali ya awamu ya tano ya Rais Dkt John Pombe
Magufuli kwa kuunga mkono juhudi zinazofanywa na taasisi hiyo.
Chapisha Maoni