Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
Image may contain: 3 peopleNa Catherine Sungura, W. Afya

WADAU mbalimbali wa sekta ya Afya wametakiwa kufanya juhudi katika  kuimarisha  afya ya mama mjamzito na mtoto nchini ili kupunguza idadi ya vifo na kujenga taifa imara.
 
Image may contain: 3 people, people sitting and table
Hayo yamesemwa jana  na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu wakati  wa ufunguzi wa mkutano wa 24 wa Wanasayansi wa ( AGOTA) uliofanyika jijini Dar es salaam .
 
Image may contain: 6 people, people sitting, table, crowd and indoor
Waziri ummy amesisitiza kuwa  vifo kwa wanawake wenye ujauzito bado ni tatizo sugu nchini, ambalo linahitaji jitihada na nguvu zaidi kupambana nalo ili kutokomeza kabisa tatizo hilo Tanzania.
 Image may contain: 5 people
“Naishukuru taasisi ya AGOTA kwa jitihada inazofanya  ikiwemo  kuhamasisha  uzazi wa mpango,kufanya  tafiti mbali mbali,  kushauri  na utoaji  huduma ya Afya  kwa mwanamke” alisema Waziri Ummy.
 
Image may contain: 1 person, suit
Kwa upande wake  Rais  wa AGOTA Prof. Andrea Barnaba  Pembe ametoa pongezi kwa Waziri  Ummy Mwalimu kutokana na jitihada anazoendelea kufanya kupitia Serikali ya awamu ya tano ya Rais  Dkt John Pombe Magufuli kwa kuunga mkono juhudi  zinazofanywa na  taasisi hiyo.Image may contain: 3 people, people standing

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement