WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu amekutana na mwakilishi Mkazi wa Shirika la Afya Duniani nchini Tanzania, Dk. Matheau Kamwa aliyemtembelea katika ofisi yake ndogo ya Wizara iliyopo Jijini Dar es Salaam.
Dkt.Kamwa amefika kujitambulisha kufuatia kuteuliwa kwake kuwa mwakilishi Mkazi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) hapa nchini.
Katika mazungumzo yao Mwakilishi mkazi wa WHO aliishukuru Serikali kwa ushirikiano uliopo katika ya WHO na Serikali na ameahidi kudumisha ushirikiano huu.
Dk. Kamwa anachukua nafasi iliyoachwa na Dk. Rufaro Chotara aliyehamishiwa nchini Afrika ya Kusini mwaka jana.
Chapisha Maoni