Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
JUMUIYA ya Maimamu Zanzibar (JUMAZA) itaazisha chuo maalum Visiwani zanzibar
kwa ajili ya wana ndoa ili kuepuka kuongezeka talaka na vitendo vya ukatili wa kijinsi.
Akizungumza na mwandishi wa blog hii, Katibu Mtendaji wa Jumuiya hiyo Visiwani hapa
Muhidin Zubeir Muhidin, alieleza kuwa chuo hicho ni kwa wazanzibari wanaotaka kuingia au waliomo ndani ya ndoa ili kujenga familia zenye maadili bora.
Alieleza kuwa chuo hicho kiko hatua za mwisho mtaala umo kwenye hatua za
kupitiwa na Afisi ya kadhi Mkuu ili kipata baraka za serikali.
“Jengo tayari tunalo ambalo linataka kufanyiwa marekebisho kidogo ambayo
yatagharimu kiasi cha milioni 10.(10,000,000)” alieleza Ustadhi
Muhidini.
Alisema kuwa Chuo kitasaidia sana
kupunguza matatizo ya wanandoa na kuleta kutengamaa vyema kwa familia na
kitasaidia sana kuondoa udhalilishaji wa kijinsia.
“Mfano talaka ni halali lakini vipi inatolewa, na Jee ikishatolewa watoto watahudumiwa na nani, hayo yote tutayasomesha kwa kina ili
kupunguza au kuwa na talaka zenye kufuata taratibu na siyo mtu kuamka
akatoa talaka” alieleza Muhidini.
Zanzibar imekuwa ikikumbwa na mrundiko wa talaka kwana na ndoa hasa vijana wanao owa na kuolewa siku hizi za karibuni.
Alieleza kuwa pia chuo hicho kitasaidia kupunguza ama kuondoa kabisa tatizo la ukatili wa Kijinsi.
Licha ya Udogo wake Zanzibar inakadiriwa na kutolewa talaka ama kwa
kupitia majumbani au kwa Mahakama ya Kadhi zaidi ya 2000 kwa mwaka.
Chanzo:maishanihabari.blog
Chapisha Maoni