Na Mwandishi Maalum
Mwanamuziki mmoja nchini Afghanistan
amelichoma rinda lake linalofanana na ngozi yake hadharani baada ya
viongozi wa dini na raia kumkosoa kwa kulivaa wakata wa tamasha moja
la hivi karibuni.
Aryana Sayeed alichapisha kanda ya video katika mtandao wa facebook akionyesha rinda hilo linavyochomeka baada ya kuzua hisia Afghanistan.
Rinda hilo la kubana alilolivaa katika tamasha mjini Paris mwezi Mei tarehe13 lilishutumiwa na viongozi wa dini pamoja na mitandao ya kijamii huku watu kadhaa wakisema kuwa linakiuka utamaduni wa Aghanistan.
Hakufurahia kulichoma rinda hilo akiwaambia zaidi ya wafuasi wake milioni 1.6 kwamba ''iwapo munafikiri kwamba tatizo kubwa nchini Afghanistan ni rinda hili nitalichoma hii leo kwa sababu yenu''.
Bi Sayeed ni mtu maarufu nchini Afghanistan, akiwa mwanamuziki, mwandishi wa nyimbo, muigizaji katika runinga anayeimbia nyimbo za Hip hop na nyimbo za Afghanistan.
Pia ni mmojawapo ya majaji wa kipindi cha vipaji vya muziki kinachopeperushwa hewani na runinga ya Tolo yenye makao yake huko Kabul.
Chanzo: BBC Swahili
Chapisha Maoni