Meneja Miradi kutoka Social Action Trust Fund (SATF) Rogasian
Massue akimkabidhi leo mfano wa hundi ya shilingi milioni 10 Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi
fedha ambazo zitatumika kwa ajili ya kulipia gharama za upasuaji wa
moyo kwa watoto watano.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Prof. Mohamed Janabi akimshukuru Meneja Miradi kutoka Social Action
Trust Fund (SATF) Rogasian Massue mara baada ya kumkabidhi leo mfano wa
hundi ya shilingi milioni 10 fedha ambazo zitatumika kwa ajili ya
kulipia gharama za upasuaji wa moyo kwa watoto watano.
Meneja Miradi kutoka Social Action
Trust Fund (SATF) Rogasian Massue akimsalimia mtoto Goodluck Msele
ambaye amefanyiwa upasuaji wa moyo hivi karibuni katika Taasisi ya Moyo
Jakaya Kikwete (JKCI) na hali yake inaendelea vizuri. SATF imechangia
shilingi milioni 10 fedha ambazo zitatumika kwa ajili ya kulipia gharama
za upasuaji wa moyo kwa watoto watano.
Daktari Bingwa wa upasuaji wa
Moyo kwa Watoto na Mkuu wa Idara ya Upasuaji wa Moyo kwa Watoto wa
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Godwin Sharau (katikati)
akimwelezea Meneja Miradi kutoka Social Action Trust Fund (SATF)
Rogasian Massue (kushoto) kuhusu aina mbalimbali za magonjwa ya moyo
yanayowasumbua watoto wanaotibiwa katika Taasisi hiyo. Kulia ni
Msimamizi wa Wodi ya watoto Afisa Muuguzi Rogers Kibula.
Meneja
Miradi kutoka Social Action Trust Fund (SATF) Rogasian Massue
akimsikiliza Daktari Bingwa wa upasuaji wa Moyo kwa Watoto na Mkuu wa
Idara ya Upasuaji wa Moyo kwa Watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) Godwin Sharau wakati akimuelezea jinsi upasuaji wa moyo
unavyofanyika katika Taasisi hiyo.
Picha na JKCI
Chapisha Maoni