moja

Responsive Advertisement
https://s-media-cache-ak0.pinimg.com/originals/c9/be/f7/c9bef7acfe128210c5f63fe803c4a2c3.jpg

NA VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM.

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Pedro Pallangyo amesema watoto wadogo nao huugua shinikizo la juu la damu.

Akizungumza na mtandao huu hivi karibuni, alisema mara nyingi hali hiyo hutokea iwapo wanakuwa wamepata magonjwa mbalimbali ikiwamo saratani.

Daktari huyo ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Utafiti na Mafunzo wa JKCI alifafanua "Tatizo hili limegawanywa katika makundi mawili kuna ‘primary hypertension’ na ‘secondary hypertension’. 

"Tunaposema ‘secondary hypertension tunamaanisha kwamba kunakuwa na kisababishi kingine ambacho kinapelekea mtu kupata shinikizo la juu la damu," alisema.

Dk. Pedro alisema “Kwa mfano saratani au mvurugiko wa homoni kwenye damu na mara nyingi hii ndiyo ambayo huwakumba watoto na kusababisha kupata shinikizo la juu la damu.

Alisema “Lakini tunaposema ‘primary hypertension’ mara nyingi huwakumba zaidi watu wazima, yaani hapa tunampima mgonjwa lakini tunakuta hakuna tatizo lolote ambalo limesababisha wao kupata shinikizo la juu la damu. Asilimia 95 ya pressure zote ni primary hypertension.

Alisema hata hivyo watoto ni nadra mno kupata tatizo hilo na kwamba kwa mwaka huwa wanawapokea watoto watano wenye shinikizo la juu la damu ikilinganishwa na watu wazima 400 hadi 500 ambao hufika katika taasisi hiyo wakisumbuliwa na shinikizo la juu la damu.

Kumbuka: Kwa mujibu wa Katiba umri wa watoto ni kuanzia mwaka 0 hadi miaka 17

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement