Na Mwandishi Maalum, W-Afya
KATIBU Mkuu Wizara ya Afya, Dk. Mpoki Ulisubisya (mwenye miwani) amewahasa wafanyakazi wa
Wizara hiyo kujiepusha na vitendo vya kupokea rushwa pindi watoapo
huduma kwa wananchi.
Dk. Mpoki ametoa rai hiyo alipozungumza kwenye kikao cha uzinduzi wa
baraza jipya la wafanyakazi wa wizara ya Afya,Maendeleo ya
Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto.
Dk. Mpoki akiongoza wajumbe kuimba wimbo wa mshikamano
Kikao hicho kimefanyika leo jijini Dar es salaam, katika ofisi ndogo ya wizara hiyo.
Kikao hicho kilihudhuriwa na wajumbe wote wa baraza hilo.
Chapisha Maoni