Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
http://www.savethechildren.org.uk/sites/all/themes/freshlime/ui/stc_logo.pngNa Veronica Romwald, Dar es Salaam

Shirika la Kimataifa la Save the Children limwakutanisha jijini Dar es Salaam zaidi ya vijana 100 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara na Visiwani,

Mkutano huo wa siku tatu unafanyika katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Nyerere  (JNICC), ambapo vijana hao watajadili na kutoa mapendekezo yatakayoiwezesha serikali kuweka mikakati yenye manufaa kuboresha afya ya vijana na Taifa kwa ujumla.

Akizungumza wakati akifungua mkutano huo wa siku tatu, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu, Jenista Mhagama amesema “Vijana ndiyo kundi kubwa kuliko makundi yote nchini, kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 inaonesha wapo milioni 16.2 kati ya watu milioni 44.

“Kwa mujibu wa Utafiti wa Nguvu Kazi uliofanywa mwaka 2014 ulionesha watu wenye uwezo wa kufanya kazi ni takriban milioni 25 na nguvu kazi inayojishughulisha na shughuli za kiuchumi ni vijana kati ya umri wa miaka 15 hadi 35 sawa na asilimia 56,” amesema.

Amesema serikali ipo tayari kupokea mapendekezo yatakayotolewa katika mkutano huo kwani yatasaidia kuboresha sera mbalimbali zinazowalenga vijana.

“Tunawahitaji kwa Tanzania ya viwanda, hatuwezi kujenga Tanzania ya viwanda ikiwa vijana wana afya duni, tunahitaji maoni yenu yatusaidie kuboresha sera zinazowalenga vijana kwa mustakabali wa Taifa,” amesema.

Makamu wa Rais wa Shirika la Global Health Save the Children (USA), Robert Clay amesema “Tafiti zinaonesha vijana ni kundi kubwa pia duniani, vijana ni Taifa la leo, mmepewa nafasi itumieni vema kutoa mawazo yenu.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement