Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


http://www.dbxdrones.com/wp-content/uploads/2016/03/google_drone.jpgPicha na mtandao

Na Mwandishi Maalumu, Dar es Salaam

Serikali imekusudia kusafirisha dawa, chanjo na nyaraka mbalimbali kwa kutumia ndege maalumu zisizotumia rubani kufikisha huduma haraka kwa wananchi.

Hatua hiyo imekuja baada ya serikali kusaini mkataba na kampuni ya Zipline ya nchini Marekani.

Katibu Mkuu (Afya) wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mpoki Ulisubsya amesema hayo Dar es Salaam wakati wa utiaji saini mkataba huo kati ya Bohari Kuu ya Dawa (MSD) na kampuni hiyo.

Dk. Mpoki amesema ndege hizo zitatumika kusafirisha dawa katika vituo vya afya, hospitalini na zahanati zisizofikika kwa urahisi.

“Tunatarajia kuanza rasmi mradi huu, mwakani katika mkoa  wa Dodoma katika vituo vya afya 200 mkoani humo ambavyo havifikiki kirahisi,” amesema.

Amesema baada ya kuanza kwa utekelezaji wa mradi huo, Taasisi ya utafiti ya  ifakara itafanya utafiti kubaini matokeo ya mradi huo na kutoa mapendekezo kama una matokeo mazuri ili kusaini mkataba mwingine wa mikoa kumi ya hapa nchini.

"Wananchi 10,000 na vituo vya afya  10000 katika mikoa yote itakayopita Mradi huu watanufaika, ikiwemo mikoa ya Kanda ya Ziwa, Pwani na Nyanda za Juu kusini,” amesema.

Ameongeza “ Katika mwaka huu wa fedha serikali iliongeza fedha katika bajeti yetu hivyo tunajipanga kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya na kuweza kufikia jamii iliyopo pembezoni mwa nchi.

Mkurugenzi Mtendaji wa MSD, Laurean Bwanakunu amesema mradi huo pindi utakapoanza utasaidia kuokoa maisha ya watu kwani dawa zitafika kwa wakati hata maeneo yenye miundombinu mibovu.

“Serikali kwa kushirikiana na MSD imeweka mikakati kuhakikisha inatoa huduma kwa jamii kwa karibu ili kuweka kuvifikia vituo vya afya zaidi ya 5,640a vilivyo chini ya  mashirika ya dini na vingine vilivyoingia mkataba na serikali kwa kutoa huduma kwa wananchi,” amesema.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Zepline Keller Rinaudo amesema ndege hizo zitakuwa na uwezo wa kubeba mzigo wa dawa au nyaraka zenye kilogramu 1.8 kwa safari moja.

Amesema pia zitakuwa na uwezo wa kusafirisha kilometa 150 kwenda na kurudi na kuahidi kampuni yake itahakikisha inatoa ajira nchini kwa vijana wengi na kuboresha huduma hiyo ili ifanyike kwa urahisi zaidi.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement