Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


005Mkuu wa Idara ya Watoto, Dk. Merry Charles akisisitiza jambo huku akionyesha kitabu hicho ambacho kitakuwa kikitumika wakati wa kuwahudumia watoto hao.

 NA VERONICA ROMWALD - DAR ES SALAAM

HOSPITALI ya Taifa Muhimbili (MNH) imezindua mwongozo maalum utakaotumika kuhudumia watoto wachanga wanaozaliwa na matatizo mbalimbali hata katika hospitali nyinginezo nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jana wakati wa hafla ya uzinduzi huo, Daktari Bingwa wa Watoto Wachanga wa Muhimbili, Edna Majaliwa alisema mwongozo huo umetengenezwa ili kuendana na hali ya sasa kwani ule ulipo umepitwa na wakati.
 002
Madaktari na wauguzi wakiwa kwenye mkutano wa kuzindua kitabu kinachoelezea jinsi ya kuwahudumia watoto wachanga baada ya kuzaliwa.

 “Tulikuwa na mwongozo lakini ulitengenezwa miaka mingi iliyopita, tukaona tunahitaji mwongozo mpya ambao ndiyo huu tunaozindua leo (jana), Kwa kuwa Muhimbili ni hospitali ya rufaa na tunapokea wagonjwa wengi kutoka katika hospitali mbalimbali.

“Hivyo, tuliona tunahitaji kama Taifa kuwa na mwongozo wa pamoja ambao utasaidia kutuongoza katika kuhudumia watoto wachanga wanaozaliwa na matatizo mbalimbali,” alisema.

Alisema takwimu zinaonesha watoto wachanga wamekuwa wakizaliwa na matatizo mbalimbali huku wengine wakiwa hawajatimiza umri wa miezi tisa kama inavyopaswa.
 001
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru akizungumza katika uzinduzi wa kitabu hicho

 “Kuna visababishi vingi vinavyochangia hali hiyo kwa mfano chanzo kikuu tunaona ni maambukizi katika njia ya mkojo (hasa U.T.I), kifafa cha mimba, uzazi wa pacha, shinikizo la damu, kisukari na magonjwa mengineyo,” alisema.

Aliongeza “Hivyo ni vizuri mama kuwahi kliniki pindi tu anapojihisi kuwa ni mjamzito ili afanyiwe uchunguzi na kupewa ushauri unaostahili ili aweze kujifungua mtoto mwenye afya njema.

Naye, Mkurugenzi wa Muhimbili, Profesa Lawrence Museru alisema “Hospitali kubwa kama Muhimbili ni vizuri ikiwa na miongozo ya namna hii hata nchi za ulaya wenzetu wana miongozo inayowasaidia kuwaongoza katika kutoa matibabu mbalimbali.

MWISHO

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement