Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
*Ni sehemu ya maadhimisho Siku ya Moyo Duniani yanayofanyika kila mwaka Septemba 29, mwaka huu (kesho)

NA MWANDISHI MAALUMU - DAR ES SALAAM

WITO umetolewa kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam na maeneo jirani kujitokeza kwa wingi, kufika katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambapo leo watatoa elimu ya lishe, jinsi ya kujikinga na magonjwa ya moyo.

Rai hiyo imetolewa leo na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi hiyo, Tulizo Shemu alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu Maadhimisho ya Siku ya Moyo Duniani yanayofanyika kila ifikapo Septemba 29, kila mwaka (kesho).

“JKCI tumekusudia kufanya upimaji wa magonjwa ya moyo kwa kila mtu ambaye atafika kesho (leo) kuanzia saa mbili hadi saa 10 jioni bila gharama yoyote, kuanzia Septemba 25 hadi 29, mwaka huu tayari tumewafanyia upasuaji wagonjwa 23 kwa kushirikiana na madaktari wenzetu kutoka Taasisi ya Madaktari Afrika,” amesema.

Amesema JKCI wanafanya maadhimisho hayo kwa kushirikiana pia na Chama cha Madaktari wa Moyo Tanzania (THF).

“Wananchi watapimwa urefu, uzito, shinikizo la damu (BP), sukari na  kupewa ushauri. Kwa wale watakaokutwa na matatizo ya moyo watafanyiwa uchunguzi zaidi na kupatiwa matibabu. Kauli mbiu ya siku hii ni:  “Moyo wenye Afya”,” amebainisha.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement