Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement

Na Veronica Romwald, Dar es Salaam

WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu  ameziagiza hospitali zote zilizopo chini ya serikali zikiwamo za Kanda, za Mikoa, Wilaya, zahanati na vituo vya afya kote nchini kuhakikisha zinatenga siku maalumu kwa ajili ya kufanya upimaji wa saratani ya matiti na kizazi.

Agizo hilo amelitoa Dar es Salaam leo wakati alipozungumza wakati alipokuwa akifunga matembezi ya hisani ya kuhamasisha uchunguzi wa saratani ya matiti na saratani ya shingo ya mlango wa kizazi katika viwanja vya Taasisi ya saratani Ocean Road (ORCI).

Waziri Ummy amesema tatizo la saratani linazidi kuongezeka ambapo kila mwaka takriban wagonjwa wapya 50,000 hugundulika.

"Inakadiriwa ifikapo 2020 idadi ya wagonjwa wa saratani itaongezeka mara mbili ya wagonjwa wapya na kufikia wagonjwa 100,000 ikiwa hatua hazitachukuliwa, "amesema.

Amesema hali inaonesha wagonjwa wanaofika hospitalini kwa uchunguzi ni asilimia 26 pekee na kwamba katika wagonjwa 100 wagonjwa 74 hawajulikani wanapopata tiba na uchunguzi huku asilimia 80 ya wagonjwa hufika wakiwa katika hatua za mwisho na kusababisa matibabu kutokuwa mazuri.

Amesema serikali imeongeza kiwango cha upatikanaji wa dawa katika taasisi hiyo mara nne zaidi ya ilivyokuwa awali.

"Awali upatikanaji wa dawa ulikuwa kiwango cha asilimia nne tu kwa sababu bajeti iliyokuwa ikitengwa ilikuwa ndogo walikuwa wanapokea Sh milioni 790 lakini tumeiongeza hadi Sh bilioni saba.

Amesema serikali imekusudia kabla ya Juni 30, 2018 kununua kipimo cha kisasa cha uchunguzi wa magonjwa ya saratani cha PET/CT Scan.

"Tumetenga Sh bilioni 14.5 kwa ajili ya ununuzi wa kifaa hicho tutakapofunga Tanzania itakuwa nchi ya kwanza Afrika Mashariki na Kati," amesema.

Akizungumza Mkurugenzi Mtendaji wa ORCI, Dk. Julius Mwaiselage amehimiza jamii kuwa na utamaduni wa kufanya upimaji mara kwa mara kwani saratani ikigundulika mapema hutibika na kupona kabisa.

"Asilimia 80 ya wagonjwa wanaofika hospitalini huwa wamechelewa, ili kuwasaidia zaidi wagonjwa tunaowapokea, kupitia matembezi tuliyofanya miaka ya nyuma tumeweza kuboresha wodi za saratani na tumeongeza idadi ya vitanda kutoka 40 hadi 100 katika chumba cha chemotherapy, hatua hii imesaidia wagonjwa kupata huduma kwa wakati na kwa muda mfupi," amesema.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement