Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Koo, Pua na Sikio wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Edwin Liyombo akiwaonesha waandishi wa habari kifaa cha coclea implant ambacho hupandikizwa kwa watoto waliozaliwa na tatizo la usikivu (picha na Veronica Romwald).

Na Veronica Romwald, Dar es Salaam
 
HOSPITALI ya Taifa Muhimbili (MNH) inatarajia kufanya upasuaji wa awamu ya pili, kupandikiza vifaa vya usikivu kwa watoto waliozaliwa na tatizo la kutokusikia (ukiziwi).

Akizungumza na mtandao huu, mwishoni mwa wiki Ofisa Uhusiano wa hospitali hiyo, Neema Mwangomo alisema tayari watoto sita wameandaliwa kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji huo.
 http://mtanzania.co.tz/wp-content/uploads/2016/11/Neema-Mwangomo.jpg
Mwangomo (pichani) alisema upasuaji huo utafanywa na wataalamu wa Muhimbili kwa kushirikiana na wataalamu wenzao kutoka kampuni ya MEDEL ya nchini Austria.

“Tunatarajia upasuaji huo utafanyika Novemba, mwaka huu...hatua hii ni muendelezo Wa jitihada tunazofanya za kutoa huduma za kibingwa na kupunguza rufaa kwa wagonjwa wanaotakiwa kwenda kutibiwa nje ya nchi,” alisema.

Mwangomo alisema gharama za upasuaji kwa kila mtoto anayehitaji kuwekewa kifaa cha usikivu ni milioni 36 pekee hospitalini hapo.

“Wakati akipelekwa nje ya nchi kwa matibabu huwa inagharimu takriban Sh milioni 80 hadi Sh milioni 100 kwa mtoto mmoja,” alisema.

Aliongeza “Kwa hiyo kuwapo kwa huduma hii hapa Muhimbili inasaidia kupatikana kwa gharama nafuu zaidi na hivyo kuwezesha watoto wengi kupatiwa huduma hiyo ya matibabu.
 https://hearnet.org.au/wp-content/uploads/2015/10/Hyrbid-CI.png
Kifaa cha cochlea implant

Alisema hatua hiyo itachochea pia kuwapo kwa mawasiliano kwa watoto na wazazi wao na kupata elimu anayohitaji hivyo kupunguza mzigo kwa familia na jamii kwa ujumla.

“Huduma hii ilizinduliwa Juni 7, mwaka huu na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, kwa hatua hiyo Tanzania imekuwa nchi ya kwanza kutoa huduma hiyo katika hospitali za umma na ya pili katika Ukanda wa Afrika Mashariki ikitanguliwa na Kenya,” alisema.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement