Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement

https://famespy.files.wordpress.com/2009/07/mj-gold-coffin.jpg?w=500Na Veronica Romwald, Dar es Salaam

WAKILI wa Mahamaka Kuu Tanzania, Maulid Kikondo amesema kifo chochote kinapotokea kwa kutatanisha ni lazima uchunguzi ufanyike kabla ya mwili wa marehemu kuzikwa.

Amesisitiza ni makosa ndugu kufanya maziko bila kupata taarifa ya daktari inayoeleza sababu iliyopelekea kifo hicho kutokea.

Wakili Kikondo amesema hayo alipozungumza na matukionamaisha katika mahojiano maalumu ikiwa ni muendelezo wa mazungumzo kuhusu Sheria ya Matibabu.

“Kosa kubwa ambalo naona watu wengi wamekuwa wakilifanya ni kuogopa au kukwepa kuhudhuria kipindi mwili wa marehemu unapokuwa unafanyiwa uchunguzi,” amesema.

Amesema kitendo hicho kinasababisha kushindwa kujua nini hasa kimepelekea kifo chake iwapo ni uzembe uliotokana na wataalamu wa afya au la.

“Matibabu yanapaswa kuwa professional, kwa mfano unapomfikisha mgonjwa wako hospitalini akapoteza maisha ndani ya saa 24 akipatiwa matibabu ni lazima mjue nini kinasababisha kifo chake.

“Lakini bahati mbaya, watu wengi huogopa kuhudhuria kwenye 'postmotum' matokeo yake ni kwamba hamtajua ukweli kuhusu kifo hicho,” amebainisha.

Ameongeza “Ikiwa kimesababishwa na uzembe wa daktari, kwa kuwa mmeogopa anaweza kutumia mwanya huo kutengeneza taarifa isiyo ya kweli na ninyi makosa hali ya ndugu yenu.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement