Na Mwandishi Maalumu, Dar es Salaam
MTOTO mwenye umri wa miezi tisa amefanyiwa upasuaji kutibu tatizo la moyo linalomsumbua katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).
Matibabu hayo yamefanyika katika kambi ya matibabu inayoendelea hospitalini hapo iliyoanza mapema jumatatu wiki hii.
Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi ameudokeza mtandao huu mapema jioni kwamba moyo wa mtoto huyo upo upande wa kulia.
*Ikumbukwe kwa kawaida moyo wa binadamu upo katika upande wake wa kushoto na si kulia.
Amesema upasuaji huo umefanyika kwa mafanikio makubwa.
Mkurugenzi huyo amesema mapema kesho watatoa taarifa kwa kina kuhusu upasuaji huo wa kihistoria uliofanyika hospitalini hapo.
Amesema upasuaji huo umefanyika kwa mafanikio makubwa.
Mkurugenzi huyo amesema mapema kesho watatoa taarifa kwa kina kuhusu upasuaji huo wa kihistoria uliofanyika hospitalini hapo.
Chapisha Maoni