Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgGxi4l5-rEort3Gq_lSm6mnpLy2S-LwTGKQxqbtyXm8eXs1qxQrV_UzdZfmYkLFcx2cRK-IB6pCR3gxLGL1chwx19HQdUL4zIGxoS8MBMLFDWNgwlAUoeE2g2eYRgynuIuHqdv_-jXHlJg/s640/9.jpgNa Veronica Romwald, Dar es Salaam

TAASISI ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu Muhimbili (MOI) inakabiliwa na uhaba wa vyumba vya upasuaji ili kutosheleza mahitaji yake.

Akizungumza jana hospitalini happy  wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kujitolea Duniani ambapo pia alipokea msaada was fedha  na vifaa mbalimbali  kutoka Taasisi ya Foundation for Civil Society, MkurugenziBoniface alisema hivi sasa wanavyo vyumba sita pekee.

"Kwa taasisi hi tunahitaji kuwa navyo angalau 15 ili kutosheleza na pia tunatamani tungekuwa na chumba kimoja kwa ajili ya watoto pekee, asilimia 60 ya wagonjwa wetu huhitaji upasuaji," alisema.

Alisema kutokana na hali hiyo wanalazimika kufanya upasuaji kwa watoto wenye tatizo la kichwa kikubwa na mgongo wazi hasa jumamosi.

"Huwa tunawafanyia Kati ya watoto 20 hadi 50 kwa siku na wakati mwingine tunalazimika kufanya hadi usiku," alisema.

Aliishukuru serikali kwa kuendelea kuijengea uwezo taasisi hiyo pamoja na wadau mbalimbali wanaoendelea kusaidia ukiwamo Ubalozi was Kuwait nchini.

"Serikali ina nia ya dhati kuboresha sekta ya afya, wadau wakiwamo Jumuiya Khoja Shia Ithna Asher nao wamekuwa wakifadhili matibabu ya watoto ambapo hadi sasa tumefanya kambi 20 na watoto 400 wamenufaika.

"Shughuli hizi ili tufanikishe tunahitaji damu ya kutosha, ubalozi wa Kuwait ulitupatia benki ya damu, hivyo natoa rai kwa wananchi kuja pia kujitolea damu ili kwa pamoja tufanikishe matibabu haya," alisema.

Dk. Boniface aliishukuru Taasisi ya Foundation for Civil Society kwa kuungana na taasisi hiyo katika kuwezesha matibabu ya watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi.

Awali, Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Francis Kiwanga alisema wapo tayari kuwakatia bima ya afya  watoto 50 wenye matatizo hayo wanaotibiwa hospitalini hapo.

"Leo (jana) tunakabidhi pia msaada wa vitu mbalimbali wenye thamani  ya zaidi ya Sh milioni 15 ikiwamo mchele, mafuta ya kupikia, sabuni za kuogea, nepi za kisasa (parmpas), mafuta ya kupaka, magodoro na vinginevyo.

"Pamoja na hivyo, tunakabidhihundi yenye thamani ya Sh milioni nane zitakazowezesha matibabu ya upasuaji kwa watoto 100 wenye tatizo hilo," alisema.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement