Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
Image may contain: 4 people, people smilingNa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Mpoki Ulisubsya akimsikiliza daktari wakati wa ziara yake hiyo.

Mwandishi Maalum, Dar es Salaam

Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Upasuaji wa Ubongo ,Mgongo na Mishipa ya Fahamu (MOI) imeokoa zaidi ya shilingi Bilioni 5 ambazo zingetumika kusafirisha wagonjwa nje nchi kufuataia kuanzisha huduma za kibingwa ambazo awali zilikua hazipatikani hapa nchini.
Image may contain: 7 people, people smiling
Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya , Maendeleo ya Jamii , Jinsia Wazee na watoto Dkt Mpoki Ulisubisya alipofanya ziara katika taasisi hiyo ili kujiridhisha shughuli za utoaji huduma katika taasisi hiyo.
 
Image may contain: 1 person, sitting

Akizungumza na menejimenti ya MOI Dkt Ulisubisya amepongeza kazi nzuri na kubwa inayofanywa ambayo imepelekea watanzania kupata huduma bora za kibingwa ambazo wangepaswa kuzifuata nje ya nchi.
 
Image may contain: 1 person, sitting
"Mnafanya kazi nzuri sana , jambo ambalo linatupa faraja kubwa sisi viongozi wenu, naomba muongeze ubunifu zaidi. Hamtakiwi kuifikiria MOI kwenye ukanda huu wa Afrika pekee bali duniani. Hii ni changamoto kwetu sote kuifikisha hapo," amesema Dkt Ulisubisya.Image may contain: 19 people, people smiling, people standing and outdoor

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement