Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
Picha na mtandao

NA VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM

WAKATI baadhi ya ndugu wa wagonjwa  wanaolazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) wakilalamikia kitendo cha kulipisha faini ya Sh 50,000 pindi wanapokutwa wamekaa juu ya vitanda vya wagonjwa.

Uongozi wa Hospitali hiyo umesema haujawahi kupokea malalamiko yoyote kuhusu suala hilo.

Mmoja wa ndugu aliyelazwa hospitalini hapo ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini alilieleza MTANZANIA kwamba kitendo hicho kimekuwa kikifanyika katika jengo la watoto lililopo hospitalini hapo.

“Imekuwa kero kubwa, kuna wauguzi ambao ukikaa kwenye kitanda cha mgonjwa wanakuchukua na kukudai faini ya Sh 50,000, inatushangaza kwa sababu hakuna tangazo lolote la hospitali lililobandikwa kutoa onyo lolote.

“Ukikaa tu unashtukizwa, unachukuliwa na kwenda kulipishwa faini hiyo… na hakuna kiti angalau kimoja angalau mtu aweze kukaa wakati akimuuguza ndugu yake,” alidai.
Kutokana na hali hiyo, MTANZANIA (matukionamaisha) lilimtafuta Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma na Huduma kwa Wateja, Aminiel Aligaesha (Pichani) ambaye alionesha kushangazwa na suala hilo.

“Ni uwongo, Muhimbili hatutozi faini kwa kosa la ndugu kukaa juu ya kitanda cha mgonjwa, jamii ielewe kwamba hospitali haina utaratibu huo,” alisema.

Aliongeza “Lakini ‘hatu-incourage’ (hatupendelei) ndugu wakalie vitanda vya wagonjwa kwa sababu mwisho wa siku wataondoka na ‘infections’ (maambukizi)… huku ni hospitali.

Alisema ni vigumu kuweka angalau kiti kimoja katika wodi za wagonjwa wa jumla kama ilivyo kwa wodi za VIP kwa sababu kutaongeza msongamano wa watu.

“Hatuwezi kwa sababu unakuta wodi ina vitanda 30 hadi 40 tukisema tuweke viti maana yake itabidi tuweke kulingana na idadi ya vitanda tutakuwa tumeongeza msongamano mkubwa mno ndani ya wodi.

“Hivyo, naomba ndugu yeyote atakayedaiwa kutoa kiasi hicho cha fedha ni vema aje atoe taarifa na sisi tutazifanyia kazi haraka iwezekanavyo dhidi ya muhusika,” alitoa rai.

Habari hii imeripotiwa leo kwenye gazeti la MTANZANIA ambalo nalitumikia pia


Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement