Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/7/71/Menschliches_auge.jpg/220px-Menschliches_auge.jpg
NA VERONICA ROMWALD - DAR ES SALAAM
JICHO ni sehemu ya mwili inayowezesha kuona, ni ogani inayotambua mwanga na kutuma taarifa zake kwenye ubongo.
Binadamu ana macho mawili katika sehemu ya uso wake, moja upande wa kulia na jingine kushoto.

Kila jicho la  binadamu lina lenzi moja kama ilivyo kwa viumbe wengine  waliopo katika kundi la mamalia.

Muundo wa jicho huruhusu kuona vitu mbalimbali kama vile rangi, umbali na mambo mengine mengi. 

Pamoja na umuhimu wake mkubwa kwa viumbe hai wakati mwingine macho hudhurika kwa maradhi mbalimbali.

Kutokana na maradhi mtu huweza kujikuta akipata tatizo la kuona mbali, karibu  na huono hafifu na hatimaye upofu.

Tunashuhudia katika jamii zipo familia ambazo baba, mama hadi watoto hulazimika kuvaa miwani kuwasaidia kuona karibu au mbali.

Nimemtafuta mtaalamu wa afya na magonjwa ya macho na kufanya naye mahojiano maalum.

Katika makala haya, Daktari Asha Mweke wa Kituo cha Letasi eye and Optical Centre kilichopo jijini Dar ea Salaam, anaeleza kwa kina juu ya jambo hilo.

Anasema yapo matatizo ya macho ambayo hurithiwa kutoka kizazi hadi kizazi na ikiwa wahusika huchelewa kupata matibabu huweza kujikuta wakipata upofu moja kwa moja. http://habariclouds.com/wp-content/uploads/2017/07/90ef81a19d9cd5e5eb43eb3f38cd906e-cat-eye-glasses-eye-glasses-for-women-300x300.jpg
"Yapo matatizo au maradhi ya macho ambayo yanahusiana na kurithi, kwa mfano mtoto anapokuwa hawezi kuona mbali kitaalamu inaitwa myopic...yaani anaweza kuona vitu vya karibu lakini vya mbali hawezi kuona.

"Mara nyingi huhusianishwa na kurithi na ukiangalia historia utakuta baba au mama yake lazima utakuta mmoja au wote walikuwa na tatizo hilo na huenda walikuwa wanavaa miwani," anabainisha.

Anasema myopic ndilo tatizo ambalo linahusiana na uvaaji miwani na ambalo hurithiwa kuliko matatizo mengine ya macho.

"Yaani ni tatizo la huoni hafifu ambapo mtu huwa hawezi kuona vitu vilivyopo mbali lakini vile vilivyopo karibu anaviona," anasema.

Dk. Mweke anasema yapo pia matatizo mengine ambayo hurithiwa ikiwamo tatizo la glaucoma ('pressure' ya macho) ingawa ni kwa asilimia ndogo.

"Kwa hiyo kabla ya kumtibu mgonjwa ni lazima tufuatilie historia yake na kwa yule mwenye tatizo la glaucoma lazima tuangalie kwenye familia kama kuna mtu alipata upofu bila kujitambua na mambo mengine mengi," anasema.

Anaongeza "Tatizo la glaucoma hurithiwa lakini watu wengi hawalifahamu tatizo hili na huwa  linaleta upofu lakini halina dalili na wala hauna maumivu.

"Ile 'pressure' ya macho huwa inapanda na matokeo yake huwa inaua mishipa ya fahamu (optic nerve), mishipa hiyo huanza  kufa taratibu taratibu na mtu ghafla anajikuta haoni au huoni unapotea pole pole," anasema. http://www.timepass.info/image.axd?picture=2012%2F2%2FEyes.jpg
Daktari huyo anasema hata hivyo ipo aina nyingine ya glaucoma ambayo yenyewe huja kwa ghafla na ambayo humsababishia mtu  maumivu makali mno upande mmoja wa kichwa.

"Utakuta mtu ghafla anaumwa na kichwa upande mmoja na kinakuwa kinamuuma kweli kweli na akifanyiwa vipimo anakutwa 'pressure' ya jicho lake ipo juu.

"Lakini ile ambayo ni 'chronic' yenyewe huanza taratibu na huwa haina dalili wala maumivu, huhisi chochote lakini uwezo wa kuona hupungua taratibu taratibu," anasema.

Athari yake

Anasema kitendo hicho husababisha mishipa ya pembeni ya macho kuanza kufa taratibu na hadi mtu anakuja kujigundua hukutwa tatizo limekua kubwa na pengine huoni umebaki kidogo sana.

"Huwa ana kiwango kidogo cha kuona inapofika hatua hiyo kinachofanyika....hupatiwa tiba ya kushusha ile 'pressure' lakini haitasaidia kuongeza ule uono wake.

"Hata kama atafanyiwa upasuaji, hakuna uwezekano wa kurudisha ule uoni kama tayari tatizo ishaleta athari kwenye mishipa yake ya fahamu," anasema.
 
Mtaalamu huyo akimfanyia uchunguzi mwanafunzi katika moja ya kambi za uchunguzi wanazofanya katika shule mbalimbali

Wanamsaidiaje mgonjwa

Anasema cha kwanza wanachofanya ikiwa 'pressure' ipo juu mgonjwa hupatiwa dawa ya matone ambayo huiweka kwenye macho yake kwa ajili kuishusha ili iwe sawa sawa.

"Lakini lazima pia tuangalie hiyo 'pressure' imesababishwa na nini ndipo tumtibu," anabainisha.

Siri ya kufumba na kufumbua jicho.

Daktari huyo anasema kitendo cha jicho kufumba na kufumbua (kukonyeza) husaidia kulainisha mboni ya jicho ambayo haitakiwi kuwa kavu.

“Mboni ya jicho ikiwa kavu inapata ukungu na hatimaye upofu… machozi husaidia kulainisha mboni ya jicho (cornea),” anasema.

Anasisitiza “Machozi ni muhimu kwa afya ya jicho la binadamu na huwa yanapita kwenye vifereji hadi kwenye pua.

Athari ya mishipa

Anasema kitendo hicho cha ‘pressure’ ya jicho kuongezeka husababisha athari katika mishipa ya fahamu iitwayo ‘optic nerve’.

"Zile optic nerve huanza kuathika, kwa hiyo tiba yake mgonjwa hupatiwa matone au dawa ambazo ni maalumu za kushusha ile 'pressure'.

“Ni vema mtu akawahi mapema hospitali ili ile ‘pressure’ isije ikaleta athari kwa sababu itakapoleta athari kwenye mishipa ya fahamu haitaweza kurekebishika zaidi.

“Yaani kama huoni wako ni hafifu utabaki hivyo hivyo, utapewa tiba si kwa kukufanya urudi au uweze kuona zaidi isipokuwa utabaki na huono huo huo ulionao,” anasema.

Dk. Mweke anasema tatizo ni kwamba magonjwa ya macho hatapewi Kipaumbele na jamii.

“Tunaona kwenye kliniki yetu jambo hili kwa sababu macho yenyewe si kama tumbo, tumbo linapouma 'likimsokota' mtu atakimbilia hospitali lakini kwa matatizo ya macho unakuta mtu ana-ahirisha kwenda hospitalini,” anasema.

Anasema kutokana na hali hiyo wagonjwa wengi wa macho huensa hospitalini wakati hali imeshakuwa mbaya. http://wagr.org/wp-content/uploads/2015/03/aniridic_eye.png
“Na ikishakuwa mbaya unakuta mgonjwa kwa mfano wa glaucoma hakuna kitakachomsaidia zaidi ya kushusha ile 'pressure' ikae sawa sawa.

“Tunawapatia ushauri kuhusu huoni wao na kisha tunawapatia rufaa kwenda kuwaona madaktari waliobobea kutibu tatizo la glaucoma ambako huko pia hupewa ushauri na matibabu zaidi,” anasema.

Dk. Mweke anasema katika kituo chao wanapokea wagonjwa wenye matatizo ya macho makundi yote kuanzia watoto hadi watu wazima.

“Wapo ambao wamepata kwa kurithi wengine kutokana na magonjwa mengine ikiwamo kisukari, shinikizo la damu na mengine.

“Tunashauri jamii kujenga utamaduni wa kupima afya ya macho angalau mara moja kwa mwaka hii itasaidia kubaini mapema kama wana matatizo wapate matibabu mapema,” anasema.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement