Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjk25fdNzbnsaht6BDp_EeapN7prw4NIvFETxmyDktaoQR-g1YgzummnJmb95cjx0WTKeWon6NEcHlbCNRVIUtVcOcavnSCws6M7kFbuyawyf3YbGmVDd2UV3MLpNXRwnzjmzVimWs1mak/s640/OTH_9383.JPGRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli
 
Na Mwandishi Maalum, Switzerland
 
Tanzania imetajwa kuwa nchi bora katika Bara la Afrika kwa kuwa na Uchumi Jumuishi (Inclusive Economy) katika Mkutano wa Uchumi Duniani (World Economic Forum).

Tanzania inaongoza nafasi ya kwanza ikifuatiwa na nchi ya Ghana na Cameron.

Mkutano huo ulifanyika Davos Switzerland kuanzia Januari 23 hadi 26, mwaka huu. 

https://pbs.twimg.com/profile_images/480420600306204673/-gN3oMFi.jpeg
Kupitia taarifa yake aliyoituma kwa vyombo vya habari mapema leo, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kuinua Diplomasia ya Uchumi Tanzania (TEDEF), Dk. Telesphory Kyaruzi (Pichani) amesema hatua hiyo ni kubwa na ya kupongeza.

"TEDEF tunaungana na World Economic Forum kumpongeza Rais John Magufuli kwa hatua hii, ambayo imechangiwa na serikali anayoiongoza kuhimiza watu kufanya kazi halali ili kujipatia kipato.

"Aidha, kuhimiza kila mwananchi anayeshiriki kufanya shughuli za kiuchumi kuhakikisha analipa kodi na hivyo kupata fursa sawa za kiuchumi," amesema.

Dr Kyaruzi ameongeza "Tanzania itaendelea kukua kiuchumi kutokana na maono aliyonayo Rais Magufuli hususan kufikia Tanzania ya uchumi wa kati kwa kutumia rasilimali tulizojaliwa na Mwenyezi Mungu.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement