Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
https://ippmedia.com/sites/default/files/styles/image660/public/articles/2017/02/06/UKOMA.JPEG?itok=NayVFlKv&timestamp=1486354109Picha na mtandao

NA VERONICA ROMWALD - DAR ES SALAAM

UGONJWA wa ukoma bado umeendelea kuwa tatizo la kiafya nchini ambapo idadi ya kiwango cha ugunduzi wa wagonjwa kimeongezeka.

Mwaka 2006 kiwango cha ugunduzi kilikuwa mgonjwa mmoja kati ya wagonjwa 100,000 ambacho kimeongezeka kufikia wagonjwa wanne katika watu 100,000 mwaka 2016.

Hayo yalielezwa Dar es Salaam jana na Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Faustine Ndungulile alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu Maadhimisho ya Siku ya Ukoma Duniani yanayofanyika Januari 28, kila mwaka.

"Takwimu za Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma za mwaka 2016 jumla ya wagonjwa wapya 2,047 waligundulika, takwimu hizo zinaifanya Tanzania kuendelea kuwa miongoni mwa nchi 22 zenye wagonjwa wengi wa ukoma duniani," alisema.

Alisema takribani mikoa yote nchini inagundua na kutibu wagonjwa wa ukoma japo kwa viwango tofauti.

"Hivi sasa bado kuna mikoa kumi ambayo inagundua wagonjwa wapya kila mwaka, mikoa hiyo ni pamoja na Lindi, Mtwara, Morogoro, Pwani, Tanga, Geita, Dodoma, Tabora na Kigoma," alitaja.

Alisema bado pia zipo Wilaya 20 ambazo kiwango cha ukubwa wa tatizo la ukoma kipo juu mno na kwamba bado hazijafikia lengo la utokomezaji.

"Wilaya hizo ni Liwale, Nkasi, Ruangwa, Nanyumbu, Shinyanga, Kilombero, Mafia, Pangani, Mvomero, Masasi mjini, Lindi vijijini, Kilwa, Mpanda, Nachingwea, Rufiji, Korogwe, Mkinga, Ulanga, Morogoro vijijini na Chato," alitaja.

Dk. Ndungulile alisema takwimu za miaka 10 iliyopita kuanzia 2007 hadi 2016 zinaonesha watoto wapatao 1,456 waligundulika na kutibiwa ukoma.

"Miongoni mwa watoto hao 73 waligundulika wakiwa tayari wamepata ulemavu wa kudumu, yaani wakiwa tayari wamekatika baadhi ya viungo vyao na wengine kuhitaji kutumia viungo bandia," alisema.

Alisema kauli mbiu ya mwaka huu inasema 'Tokomeza Ukoma Kuzuia Ulemavu Miongoni mwa Vijana Wetu.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement