Mkurugenzi wa Idara ya Uuguzi na Ukunga wa Wizara hiyo, Gustav Moyo akizungumza leo katika kikao hicho.
Na Veronica Romwald, Dar es Salaam
WAUGUZI wanne na Wakunga wanne watatunukiwa tuzo na
serikali ikiwa ni hatua ya kuutambua mchango wa kazi zao wanazofanya kila siku
katika kuhudumia jamii.
Watumishi hao watakabidhiwa tuzo zao na Waziri wa
Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu ambaye
anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika
Kongamano la Kisayansi la Wauguzi na
Wakunga linalotarajiwa kufanyika mkoani Dodoma April 4 hadi 7, mwaka huu.
Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi wa Idara ya Uuguzi
na Ukunga wa Wizara hiyo, Gustav Moyo alipozungumza katika semina ya siku moja
ya kuwajengea uelewa waandishi wa habari kuelekea maadhimisho ya kongamano
hilo.
“
Chapisha Maoni