Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
Related imageNA VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM

IKIWA mtoto wako ana tabia ya kukimbia kimbia, kuruka ruka bila kujali kwamba anaweza kuumia kulingana na mazingira aliyopo, unapaswa kumfuatilia kwa makini.

Imeelezwa hizo ni miongoni mwa dalili za tatizo la ajali ya ubongo ambalo linaonekana kuwakabili watoto wengi.

Mtaalamu wa Idara ya Tiba ya Utengamao na Mazoezi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dk. Rosemary Kauzeni alisema hayo hivi karibuni alipozungumza na MTANZANIA Jumamosi katika mahojiano maalum.

Alisema kila siku katika Idara hiyo hupokea watoto wapatao 20 wanaokabiliwa na tatizo hilo na watu wazima wapatao 10.

“Linawakabili pia watu wazima lakini tunaona idadi kubwa tunaowapokea ni watoto changamoto ni kwamba wazazi wengi hawana uwelewa kuhusu tatizo hili,” alisema.

Alisema inajulikana wazi watoto huwa ni wachangamfu lakini inapotokea ule uchangamfu unapitilia mzazi anapaswa kufuatilia kwa umakini.

“Uchangamfu unapopitilia si hali nzuri ni dalili za mtoto kukabiliwa na tatizo hili la ajali ya ubongo,” alisema.

Mtaalamu huyo alibainisha dalili nyingi za tatizo anazoonesha mtoto, dalili kwa watu wazima na matibabu yake.

Kujua kwa undani tafadhali usikose nakala ya gazeti la MTANZANIA alhamis wiki hii.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement