Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement

Image result for vyombo vya chakulaBaadhi ya vyombo vya kulia chakula.

NA VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM

WATU wanaogundulika kuwa na maambukizi ya ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB) wamekuwa wakinyanyapaliwa  kwenye jamii, ikiwamo kutengewa vyombo vyao maalum vya chakula.

Imeelezwa hatua hiyo huchukua kwa hofu ya kupata maambukizi ya ugonjwa huo hata hivyo dhana hiyo si sahihi kwani TB haiambukizwi kupitia vyombo vya chakula.

Akizungumza Dar es Salaam juzi katika mafunzo ya siku moja kwa waandishi wa habari za afya yaliyolenga kuwajengea uwelewa kuhusu ugonjwa huo, Mfuatiliaji wa Tathmini wa Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma, Dk. Zuweina Kondo alisema huambukizwa kwa njia ya hewa.

“Jamii bado haina uwelewa wa kutosha juu ya namna TB inavyoambukizwa, ugonjwa huu huambukizwa kwa njia ya hewa na si vyombo vya chakula.
Image result for someone coughing
Inashauriwa uwahi hospitalini kwa uchunguzi ikiwa unakohoa kwa zaidi ya wiki mbili.

“Kibaya zaidi ni kwamba mtu hutengwa pale tu anapogundulika lakini kabla ya kugundulika huwa wanashirikiana naye bila wasiwasi wowote.

“Jambo hili si sahihi, kimsingi mtu ambaye amegundulika kuwa na maambukizi na ameanza matibabu anakuwa salama na unaweza kushirikiana naye vyombo vya chakula.

“Kibaya ni kwamba mtu mwenye maambukizi ambaye hajagundulika ili kuanza matibabu ndiye anakuwa na uwezo wa kuambukiza wenzake TB,” alisema.

Alisema kitendo cha wale waliogundulika kuwa na maambukizi ambao wameingizwa kwenye mfumo wa matibabu kutengwa na kunyanyapaliwa kinafanya wengine kuwa na hofu ya kufanya uchunguzi juu ya afya zao.

“Wanaogopa watatengwa na hii ni changamoto katika mapambano dhidi ya ugonjwa huu, kulingana na Shirika la Afya Duniani (WHO) Tanzania ipo miongoni mwa nchi 30 zenye maambukizi makubwa ya TB,” alisema.

Alisema ripoti ya Shirika la Afya Duniani (WHO) ya mwaka 2017 inaeleza kiwango cha maambukizi ya TB nchini ni wastani wa watu 287 katika kila watu 100,000, sawa na wagonjwa 160,000 kila mwaka.

“Lakini ripoti yetu ya mwaka 2016 inaeleza katika mwaka huo pekee tuliweza kugundua na kuwaingiza katika mfumo wa matibabu watu 64,000 sawa na asilimia 40,” alisema.

Alisema asilimia 90 ya watu wanaogundulika kuwa na maambukizi hayo na kupatiwa matibabu mapema hupona hata hivyo changamoto ni namna ya kuipata asilimia 60 ya wagonjwa iliyobakia.

Alisema kulingana na ripoti hiyo ya WHO ya mwaka 2016 inakadiriwa ya watu bilioni mbili duniani wanaishi na maambukizi ya ugonjwa huo duniani.

“Ni ugonjwa ambao unaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa kwa upande wa magonjwa ya maambukizi (yanayosababishwa na vimelea) kuliko hata Ukimwi kulingana na WHO,” alisema.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement