Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement

NA VERONICA ROMWALD - DAR ES SALAAM

Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) inatarajia kuanza kutoa huduma ya uchunguzi wa awali dhidi ya saratani ya utumbo ambayo kwa mujibu wa takwimu inaonesha idadi ya watu wanaougua ugonjwa huo imeongezeka.

Akizungumza na MATUKIO NA MAISHA hivi karibuni ofisini kwake, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Saratani wa ORCI, Crispin Kahesa alisema saratani hiyo imepanda kutoka nafasi ya 20 kati ya saratani zenye idadi kubwa ya wagonjwa hadi kuwa miongoni mwa saratani 10.

“Tayari tumeagiza vifaa vya uchunguzi, kwa kutumia kifaa hcho tunaweza kuona dalili za awali za saratani hii kwa kupima kinyesi cha mtu husika na hivyo kuanza kumpa matibabu kwa wakati,” alisema.

Alisema miongoni mwa mambo yanayochangia mtu kupata saratani hiyo ni unywaji wa pombe kupindukia hasa zile kali na ulaji wa nyama uliopita kiasi.

“Kiujumla mfumo wa maisha unachangia kwa kiwango kikubwa mtu kupata saratani hii na hatari zaidi ipo kwa kundi la wanaume kuliko wanaume,” alisema.

Alisema vifaa hivyo vitakapowasili ORCI itatoa taarifa kwa umma lini hasa itaanza uchunguzi huo wa awali na kwamba hivi sasa inaendelea kutoa huduma mpya ya uchunguzi wa awali wa saratani ya ngozi kwa watu wenye ualbino, saratani ya matiti na kizazi.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement