Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo Stadi (VETA), Dk. Pancras Bujulu akifafanua jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari wa Klabu ya Mkoa wa Dar es Salaam (DCPC) mwishoni mwa wiki, kushoto kwake ni Mwenyekiti wa DCPC, Irene Mark.

Na Veronica Mrema – Dar es Salaam

Vijana zaidi ya 16,000 nchini wakiwamo wanaofanya kazi ya kuuza vinywaji (Bar) wamenufaika na mafunzo mbalimbali ya ufundi stadi yanayotolewa na Mamlaka ya Elimu  ya Ufundi na Mafunzo (VETA).

Yalielezwa hayo mwishoni mwa wiki na Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo, Dk. Pancras Bujulu alipozungumza kwenye semina ya siku moja kwa wanahabari wa Klabu ya Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Dar es Salaam (DCPC), kuhusu  majukumu  yanayosimamiwa na kutekelezwa na VETA.

“VETA imekuwa suluhisho la ajira kwa vijana wengi waliokosa fursa ya kuendelea na masomo katika mfumo rasmi, kundi la wanaouza vinywaji tuliamua kuwaanzishia kozi ya huduma kwa wateja ili waweze kuboresha kazi zao wakati wanapotoa huduma,” alibainisha.

Aliongeza “Waajiri wengi hupenda kuajiri vijana waliosoma hadi ngazi ya diploma, degree, masters na PhD, wale ambao hawajafikia ngazi hizo huachwa.

“Ili kukuza sekta ya viwanda ni lazima tutambue kwamba vinahitaji mafundi mahiri na wenye ujuzi wa kutosha, lengo la Mamlaka ni kuhakikisha kinakuwa chuo cha VETA kila mkoa ifikapo 2025 ili kuzalisha nguvu kazi ya kutosha,” alisema.

Dk. Bujulu alisema tayari wana mtandao mpana wa vyuo na kwamba mikoa miwili pekee iliyosalia ambako bado hakuna vyuo vya Mamlaka hiyo ni Simiyu na Songwe.

“Sasa hivi kuna miradi ya ujenzi wa vyuo vya VETA unaendelea Kagera, Geita, Rukwa na Njombe, lengo letu pia kuhakikisha kila Wilaya inakuwa na vyuo vyetu.

“Tayari kuna jumla ya vyuo 29 vinaendelea kujengwa katika Wilaya mbalimbali nchini baada ya Serikali kutenga kiasi cha Sh. bilioni 48 katika mwaka wa fedha 2019/20 kwa ajili ya ujenzi huo,” alibainisha.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo Stadi (VETA), Dk. Pancras Bujulu akiwa katika picha ya pamoja na waandishi wa habari wa Klabu ya Mkoa wa Dar es Salaam (DCPC) mwishoni mwa wiki.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement