moja

Responsive Advertisement


Na Veronica Mrema – Kigoma

Jengo la Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS – Kigoma) ambalo ujenzi wake ulisimama kwa miaka 26 hatimaye unatarajiwa kukamilika mapema ifikapo Desemba, mwaka huu, jengo linatarajiwa kuwa ndilo litakalokuwa likitumika katika uchakataji wa data za Sensa ya Watu na Makazi nchini.

Akizungumza na wananchi waliohudhuria katika Maadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika yaliyofanyika Kitaifa Mkoani hapa katika Viwanja ambako ndipo zikapokuwa ofisi za NBS, Mkurugenzi Mkuu wa NBS, Dk. Albina Chuwa (mwenye blauzi na suruali nyeusi pichani) alibainisha hayo.

Dk. Albina alisema jengo hilo ndilo litakalotumika ipasavyo na kazi yake kuu ni kukusanya na kutoa uchambuzi wa mwanzo (basic analysis) katika ngazi ya mkoa na wilaya kwa kushirikiana na watakwimu wa mikoa, wilaya na halmashauri zake pia wadau wengine.

“Tunatarajia kwamba Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 data zote zitakazokusanywa zitaletwa hapa na kazi zote zitafanyika hapa hapa hadi zitakapokamilika,” alibainisha.

Aliongeza “Leo (jana) tunapata fursa ya kukagua jengo hili ambalo ndipo ilipokuwa Idara Kuu ya Takwimu nchini mwaka 1994 ilianza ujenzi ikishirikiana na Ofisi ya Takwimu Sweden.

“Ni takriban miaka 26 sasa jengo lenye ghorofa mbili lilishindikana kumalizika kwa wakati, sote tulijiuliza ‘Kwa nini?’. Serikali ya Awamu ya Tano imeamua kwa dhati na kutoa fedha Sh. milioni 684 kumalizia ujenzi na ifikapo Desemba, mwaka huu litakuwa limekamilika,” alisema.

Alisema hilo ni jambo kubwa na deni kubwa ambalo NBS inayo kwa watakwimu kuhakikisha wanalilipa kwa kujituma zaidi kwa kutumia maarifa na juhudi na Mungu aendelee kuwatia nguvu

“Serikali kwa sasa inahitaji takwimu rasmi kwa wingi zaidi katika sekta zote kuliko ilivyokuwa jana, wana-Kigoma hili ni jengo la kwanza kujengwa katika ngazi ya Mkoa kwa Ofisi ya Taifa ya Takwimu ambayo imekuwako tangu 1947 nchini.

“Hatuna budi kumshukuru Rais. Dk. John Magufuli na kumpongeza Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango kwa kuchaguliwa na wananchi wa Buhigwe Kigoma na imani kubwa ya Rais. Magufuli aliyonayo kwa Dk. Mpango kwa utendaji kazi wake.

“Kama mnavyokumbuka Dk. Mpango alipokuja kuweka jiwe la msingi Julai, 2020 aliniagiza ‘Dk. Albina Chuwaa’ hakikisha jengo hili linakamilika na kwa ubora unaostahili, sote ni mashahidi tunaona kasi inayoendelea katika ujenzi huu na litakamilika ndani ya mwaka huu 2020,” alisema.

Alisisitiza ujenzi wa jengo hilo unafanyika usiku na mchana kuhakikisha lengo hilo linatimia kwa wakati alioagizwa na kwa ubora unaostahili.

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Samson Anga (mwenye suti ya bluu pichani) akielezwa jambo na maofisa wa NBS wakingozwa na Mkurugenzi Mkuu, Dk. Albina Chuwa.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement